Miyeyusho amchakaza Mmalawi kwa KO
Bondia Francis Miyeyusho, usiku wa kuamkia jana alilinda heshima ya Tanzania kwa kishindo baada ya kumchakaza bondia kutoka Malawi, John Masamba kwa KO.


Miyeyusho, alimpiga Masamba raundi ya tano katika pambano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Vijana, Kinondoni, Dar es Salaam.