Music | Lifestyle+Fashion | Antivirus | Love+Relationships | Business+Politics | Sport | TUMA Registrations

You are here:   HomeBusiness+Politics
| + -

Political Issues

Monday, 25 February 2013 15:13 Al News - Political Issues
Print PDF

JK atua Ethiopia kuiokoa DRC
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 23, 2013 kuhudhuria utiwaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Mpango huo unatarajiwa kutiwa saini kesho Februari 24, 2013 na Wakuu wa Nchi kutoka Ukanda wa Maziwa Makuu, ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Jamhuri ya Uganda, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Angola, Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Kongo (Brazaville), Jamhuri ya Zambia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Jamhuri ya Afrika Kusini.
Aidha, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Ban Ki Moon, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa, Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma, pamoja na wenyeviti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) watatia saini Mpango huo kama mashahidi na wadhamini.
Mpango huo una nia ya kuchangia juhudi ambazo zimefanywa na Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) katika kutafuta amani Mashariki ya Kongo na ukanda wote wa Maziwa Makuu kwa ujumla.
Mpango huo pia umetilia maanani mapendekezo muhimu yaliyokubalika baada ya mashauriano kati ya wakuu wa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

 

 
Monday, 25 February 2013 14:59 Al News - Political Issues
Print PDF

Baba wa Rais Museveni afariki dunia
BABA mzazi wa Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Mzee Amos Kaguta, amefariki dunia leo asubuhi akiwa katika Hospitali ya Taifa jijini Kampala.
Mzee Kaguta aliyefariki akiwa na umri wa miaka 96,  alilazwa hospitalini hapo tangu mapema mwezi huu akisumbuliwa na maumivu ya tumbo yaliyopelekea kifo chake.
Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu.

 
Wednesday, 20 February 2013 05:09 Al News - Political Issues
Print PDF

Harakati sawa lakini wengi wanaiota amani tuliyonayoKila Mtanzania anatakiwa kulinda amani na ustawi wa nchi yake.Viongozi wana wajibu mkubwa mno kuhakikisha hakutokei mgawanyikokati ya wananchi. Siasa, ukabila na udini, havipaswi kuzungumzwa kwamapambio hata kidogo.Ni vitu ambavyo, inatakiwa tuvikemee kwa nguvu zote. Haya mamboyanayotokea sasa hivi, wengi wanachekelea.

Yanagawa watukimakundi, wapo wanaolaani, wengine wanashangilia. Kila mmoja ajuekwamba amani tuliyonayo ikipotea, itatugharimu.Ni uzuzu kushangilia mauaji ya kidini kama yaliyotokea Geita kutokanana mnyukano kati ya Waislam na Wakristo. Hakuna salama kwenyemachafuko, kila siku tambua kwamba mapigano yanapotokea,mwathirika ni wewe na yeye, kwa maana hiyo ni wote.Ukitazama migogoro hii ya sasa kwa macho yakinifu kabisa, chanzochake ni mmomonyoko wa maadili. Watanzania siyo wastahimilivutena. Hawavumiliani, kwa maana hiyo hawaheshimiani. Tenakwendakubaya mno.Huwezi kuabudu kwa umakini na ibada yake ikawa swadakta ikiwawewe mwenyewe unaishi kwa visasi. Unapigana na jirani yako kisaanaabudu dini tofauti na yako. Au mnaparurana kwa sababu yeye nimfugaji, wewe ni mkulima.Wengine ni ukabila. Chukua yote hayo halafu yaweke ndani ya kapumoja halafu jiulize yametokea wapi? Chanzo chake ni nini? Tukitakatuishi vizuri ni lazima kila mmoja aheshimu imani ya mwenzake, akubalikabila la mwenzake.

Kanuni ya kutuongoza ni hii; Ukidharau kabila la mwenzako na lakolitadharauliwa, ukichafua madhehebu ya wengine, tambua dini yako piahaitabaki salama. Ukianza kupiga nawe utapigwa. Utaumia,mtaumizana, tutaumizana.Siasa zikiingia kwenye imani ni jambo baya mno. Tutakapoanza kuonawanaharakati wa kidini wanasahau wajibu wao wa kuwaelimishawaumini kulingania imani zao kwa kufuata njia inayompendeza Mungu,badala yake kunadi siasa ni hatari.Mwaka 2010, ulizuka mgogoro mkubwa mno. Wanasiasa na Waislam,walipinga kile kilichoitwa ni Ilani ya Uchaguzi, iliyotolewa na Baraza laMaaskofu Katoliki. Wapo waliouliza, kwani Kanisa Katoliki linatakakusimamisha mgombea wa urais mpaka litoe Ilani ya Uchaguzi?Unaweza kuyatazama haya mambo juujuu lakini ukweli ni kwambaviongozi wa dini, wana nafasi kubwa mno ya kudumisha amani ya nchi.Watanzania wote watambue hilo, serikali na viongozi wenyewe wamadhehebu yote, wanapaswa kuzingatia.Amani inapaswa kuanza ndiyo watu waweze kumuabudu Mungu.Utawezaje kufanya ibada palipo na machafuko? Huo utulivu wakuwasiliana na Mungu utaupata wapi? Kumbe misikiti na makanisa nikazi bure kama nchi itakuwa haikaliki. Waumini watapita njia zipikwenda kuabudu, ikiwa mitaani kuna kuchinjana?Usalama wetu utakuwa wapi ikiwa itakuwa tunawindana? Leo Waislamwakichoma makanisa, kesho Wakristo nao wakateketeza misikiti,mwisho tutarajie kuvuna nini? Kumbe njia nzuri ya watu kulindanyumba zao za ibada ni kuheshimu nyumba za wenzao. Ukawaharibianao watakuharibia.

Inawezekana kabisa kueneza elimu kwa njia ya kidiplomasia. Kuna njianzuri zaidi katika kutoa elimu kuliko kushambulia au kukashifu.Inawezekana kumfanya mtu wa imani nyingine, kubadili dini na kufuataimani yako endapo utaweza kumjaza ukweli na akauamini.Labda kuna kitu cha kujifunza hapa, huko nyuma ilikuwaje mpaka watuwakaishi kwa upendo na sasa yamezuka yapi? Kuna viongozi wa kidiniwamesababisha haya. Wapo viongozi wa Kikristo wamepandikizambege mbaya kwa Waislam, vilevile kuna Waislam wamestawisha chukidhidi ya Wakristo.Viongozi hao ni lazima wakemewe leo, huko tulipotoka, Mkristo naMuislam wote ni ndugu, tena wanatambulika vizuri ni kizazi chaWatanzania. Hata hivyo, vizuri tukubali kwamba kuna njia tuliziachampaka haya yanatokea leo. Tukumbuke, amani tuliyonayo wengiwanaiota.

 

 
Wednesday, 13 February 2013 05:04 Al News - Political Issues
Print PDF

Kama Makinda, Ndugai wanalivuruga bunge, dawa katiba mpya
Tupo kwenye kipindi kigumu sana. Bunge kama mhimili muhimu wa kutunga sheria na kuisimamia serikali, unapitia sintofahamu ya aina yake. Wapinzani hawaelewi na hawakubaliani na hoja za kuondolewa kwa hoja zao.
Tatizo ni vyama tu! Spika wa Bunge la Tisa, Samuel Sitta, ilisemekana uongozi wake unakinzana na serikali ambayo inaongozwa na CCM. Matokeo yake, kuna kipindi ikaelezwa anatakiwa kutimuliwa ndani ya chama, baadaye imekuwa ngumu kurudi kwenye kiti hicho, akawa waziri.
Kama Sitta alishindwa kurudi kwenye kiti chake kwa sababu ya kuonekana hakipendelei chama chama chake, maana yake Makinda naye ataishi kwa angalizo hilo. Hatataka wabunge wa upinzani waiaibishe serikali ambayo inaongozwa na CCM.

Sura iliyopo sasa ni kwamba wapinzani hawana uhuru wa kuiwajibisha serikali ikiwa wabunge wengi ni kutoka CCM, spika wa bunge na wenyeviti wote ambao husimamia vikao vya bunge, wanatokea chama hicho. Hata kama watapewa uhuru, itaonekana ni sawa na mapenzi ya mama wa kambo.
Tukio la kile kinachoonekana ni kuzimwa kwa hoja za Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia ambaye ni mwenyekiti wa NCCR Mageuzi kuhusu elimu na ya Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, vimenifanya niielekeze kalamu yangu kuandika kuhusu uhuru wa kibunge kama mhimili tunaoutaka baada ya katiba mpya.
Spika wa Bunge, Anne Makinda na naibu wake, Job Ndugai, kwa kutumia mamlaka ambayo wanayo, waliziondoa hoja hizo kufuatia ombi la Mnadhimu Mkuu wa Serikali, William Lukuvi (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu na Bunge), aliyesimama kwa niaba ya serikali, kwa nyakati tofauti kutaka hoja hizo ziahirishwe kwanza.
Mnyika na Mbatia walipingana na ombi hilo, matokeo yake Ndugai akauliza wanaoafiki na wasioafiki, majibu ya ndiyo na siyo yakasikika, naibu spika akasema waliosema ndiyo wameshinda. Wapinzani wakapingana na hilo, wakaomba muongozo, hawakusikilizwa.
Makinda na Ndugai ni wana CCM ambacho ndicho chama kinachoongoza serikali. Kwa uamuzi waliofanya, yametafsiriwa kwamba yameuzima upinzani ili kuiokoa serikali. Walichokifanya, kwa wapinzani, hakiwezi kuonekana ni uimara wao wa kusimamia sheria za kibunge, bali wanasomeka ni wababe.
Tafsiri wa wabunge wa upinzani kususia kikao cha bunge na kutoka nje ya ukumbi, maana yake wanaionesha jamii ya Watanzania kwamba wanaonewa bungeni. Binafsi siwezi kuwalaumu Makinda na Ndugai, nailaumu katiba ambayo inaminya demokrasia ndani ya bunge.
Ni usaliti na unafiki mkubwa kwa Ndugai kwenda kinyume na matakwa ya CCM wakati ndicho chama kinachomfanya aitwe naibu spika leo. Ndicho kilichompa ubunge, kadhalika anaishi kwa kutekeleza sera na ilani zake. CCM ikishindwa, madaraka aliyonayo hatapata.
Kama atabaki kuwa mbunge, maana yake atakuwa mpinzani. Badala ya kushiriki kuunda serikali, atakuwa mmoja wa wakosoaji. Hata kama siyo kushindwa kwa CCM, yanaweza kuibuka ‘majungu’ kama yale yaliyokuwa yanasemwa enzi za Sitta. Nani anataka?
Hoja za Mnyika na Mbatia zilikuwa nzuri kweli, kwa maana hakuna mtu ambaye haelewi maji ni tatizo, vilevile elimu yetu inakwenda arijojo. Tulipaswa kuzishuhudia hoja hizo zikirindima mpaka mwisho.
Kitendo cha mawaziri wa elimu (waziri na naibu wake), kushindwa kutekeleza walichoahidi kwenye kikao kilichopita, kupeleka mitaala bungeni, ni kosa kubwa ambalo wabunge waliliona.
Mbaya zaidi, walifanya hivyo kipindi wanafahamu kwamba kuna hoja binafsi ya Mbatia kuhusu elimu. Waziri wa Elimu, Shukuru Kawambwa na naibu wake, Philipo Mulugo, pengine walisahau, walidharau au walifanya uzembe, sasa watawajibishwaje ikiwa hoja ilizimwa?
Twende tukajenge bunge la kidemokrasia, dawa ni moja tu, katiba mpya itamke kwamba spika, naibu wake na wenyeviti wote, wasiwe na vyama. Hilo likiwezekana, hatutashuhudia vitimbi, badala yake tutakuwa tunawaona waheshimiwa wetu wakilumbana kwa hoja.
Hiki ni kipindi ambacho, tunatakiwa kuyasoma matukio yanayoendelea na kufanya uamuzi wa kubadili hali. Kuruhusu spika, naibu wake na wenyeviti wengine wawe wanatokea kwenye vyama, hatutashuhudia demokrasia ya kweli bungeni.
Labda nifafanue kwamba demokrasia haina maana yoyote kama haionekani ikitendeka. Hapa namaanisha kwamba spika na naibu wake hata wafanye nini kuliacha bunge liwe la kidemokrasia, wapinzani hawawezi kulikubali hilo waziwazi.


 

 
Monday, 11 February 2013 06:05 Al News - Political Issues
Print PDF

Chadema waandama, wafanya mkutano Mwembeyanga

Licha ya jeshi la polisi kukionya kisifanye maandamano, Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), leo kimefanya maandamano makubwa jijini Dar es Salaam.
Viongozi wa Chadema, Mwenyekiti, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Willibroad Slaa, Naibu Katibu Mkuu,
Zitto Kabwe na wengine, waliongoza maandamano hayo, kabla ya kufanya mkutano mkubwa kwenye
viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar es Salaam.
Mkutano na maandamano hayo, vililenga kufikisha ujumbe kwa wananchi juu ya kukataliwa kwa hoja za
upinzani bungeni hivi karibuni na kusababisha bunge lichafuke.
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ambaye ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya
Upinzani Bungeni, alipata nafasi ya kuhutubia na kuwaelezea wananchi kile hasa walichokuwa

wanakilalamikia bungeni hasa baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda na naibu wake, Job Ndugai,
kuzitupilia mbali hoja za wapinzani.
Vilevile, Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, naye aliwaeleza wananchi kile kilichotokea
bungeni na kubainisha si kweli kwamba wapinzani hawajui kanuni, bali spika, naibu na wenyeviti
wamekuwa wakitoa upendeleo kwa serikali na wabunge wa CCM.
Hoja zilizoondolewa bungeni na kusababisha mnyukano bungeni ni ile Maji ya Mnyika pamoja nay a
Elimu ambayo iliwasilishwa na Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia ambaye ni mwenyekiti wa Chama
cha NCCR-Mageuzi.

 

 
Monday, 11 February 2013 05:54 Al News - Political Issues
Print PDF

Zitto Kabwe amvaa Spika Makinda
Na Zitto Kabwe
KATIKA mkutano wa Kumi wa Bunge la Kumi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Spika wa Bunge ndugu Anna Makinda alitangaza mabadiliko kadhaa ya muundo wa Bunge katika Kamati mbalimbali za Bunge. Moja ya maamuzi ya Spika yalikuwa ni kufutwa kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma ambayo inajulikana kifupi kama POAC. Maamuzi haya yameleta sintofahamu kwa wananchi wengi na wafuatiliaji wa masuala ya Bunge na Uwajibikaji katika nchi yetu. Ni muhimu tufahamu uundwaji wa POAC ulitokana na misingi gani na kwamba Uamuzi wa Spika unarudisha nyuma maendeleo makubwa ya kujenga Bunge imara na lenye meno. Maamuzi ya Spika ni kinyume cha kanuni za Bunge, sheria ya Ukaguzi na Katiba ya nchi. Maamuzi ya Spika yanavuruga Bunge,ni ya hovyo na yanapaswa kupingwa na kila mdau wa Uwajibikaji nchini.

Baada ya Tanzania kuingia kwenye zoezi la Ubinafsishaji, mashirika mengi ya Umma yaliuzwa na mengine kufa kabisa. Wakati huo kulikuwa na chombo kinaitwa SCOPO (Standing Committee on Parastatal Organisations) kwa madhumuni ya kusimamia uendeshaji wa Mashirika ya Umma. Bunge lilikuwa na Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na kamati hiyo ilifutwa mwaka 1997 kufuatia hatua za ubanifsishaji na ukweli kwamba Mashirika ya Umma hayatakuwapo na hivyo hapakuwa na haja ya kuwapo kwa kamati hiyo. Mwenyekiti wa mwisho wa Kamati hiyo alikuwa ni Mzee William Shellukindo wakati huo akiwa Mbunge wa Jimbo la Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga.
Mwaka 2007, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alifanya mkutano wa Uwajibikaji na kueleza Taifa kuwa kimsingi Mashirika ya Umma bado yapo na mahesabu yao, kwa kuwa hayaangaliwi, ni mabaya sana nafedha za umma zinapotea. Pia alieleza kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 143(5) inamtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kutoa taarifa za Ukaguzi za Mashirika ya Umma (Public Authorities and Other Bodies). Hivyo aliomba Bunge liunde Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma ili liweze kupokea, kujadili na kutoa maelekezo kuhusu mahesabu ya Mashirika ya Umma na kusimamia ufanisi wa Mashirika ya Umma. Vile vile alishauri Kamati hiyo isimamie sera ya  Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma. Spika wa Bunge wa wakati huo, kupitia Kamati aliyoiunda chini ya Job Ndugai (wajumbe wengine walikuwa dkt Willibrod Slaa, Beatrice Shelukindo, Hamad Rashid Mohammed na Nimrod Mkono) wakaunda Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma kwa mujibu wa Kanuni za Bunge za Mwaka 2007. Kamati ya POAC iliundwa rasmi mwaka 2008 mwezi Februari. Nilipewa dhamana ya kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Kamati hii. Sababu za kuanzishwa kwa kamati ya POAC bado zipo na kimsingi sababu hizo ni za maana sana sasa kuliko ilivyokuwa kabla.
Majukumu ya POAC yaliainishwa na sehemu ya tatu ya nyongeza ya nane ya Kanuni za Bunge toleo la mwaka 2007, kanuni ya 115 (13)(a-e). Majukumu hayo ni pamoja na kushughulikia mahesabu yaliyokaguliwa ya Mashirika ya Umma, kuainisha maeneo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Umma, kutathmini ufanisi wa Mashirika ya Umma na kufuatilia utekelezwaji wa sera ya ubinafsishaji wa mashirika ya Umma. Kuanzia mwaka 2008 Mdhibiti na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali amekuwa akitoa taarifa za mahesabu ya mashirika kama Katiba ya nchi inavyomtaka na sheria ya ukaguzi ya mwaka 2008. Sheria hii imeitaja kamati ya POAC kama moja ya kamati zenye majukumu ya kuwasilisha Bungeni taarifa ya mwaka ya mahesabu ya Mashirika ya Umma.
Katika kipindi cha miaka mitano POAC imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa umahiri na kwa kweli kwa uwazi sana kuliko kamati nyingine zote za Bunge. Taarifa ya mwisho ya POAC katika Bunge iliyowasilishwa katika mkutano wa saba wa Bunge, mwezi Aprili mwaka 2012 ulipelekea kutolewa kwa hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu ambayo ilisababisha mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri. Hatua hii ilikuwa ni hatua muhimu sana katika kuweka mizizi ya utamaduni wa uwajibikaji nchini kwetu. Wakati Kamati inajiandaa na Taarifa yake ya Mwaka 2012 kwenye Mkutano wa Kumi na Moja, Spika ameivunja. Ikumbukwe maagizo ya mwisho ya Kamati ya POAC yalikuwa ni kuzuia mifuko ya hifadhi ya jamii kutoa mikopo kwa Serikali bila ya kuwapo kwa mikataba. Hivi sasa Serikali imekopa zaidi ya shilingi 1.2 trilioni kutoka mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa ajili ya miradi mbalimbali, mikopo hiyo ya fedha za wafanyakazi haina mikataba yeyote na POAC iliona hatari ya fedha za wafanyakazi kupotea na kuleta madhara makubwa kwa wastaafu nchini.
Katika maelezo yake Spika amesema nchi nyingine duniani hazina kamati kama ya POAC. Nadhani waliomshauri Spika waliamua kumdanganya na yeye akadanganyika. Nchi zote za Afrika Mashariki zina Kamati ya kusimamia Mashirika ya Umma. Kenya inaitwa Public Investments Committee, Uganda inaitwa State Corporations Committee na hata nchi nyingine kama India ambazo zinafuata utamaduni wa kibunge kama wetu wanayo na wanaita Public undertakings Committee. Nchini Afrika Kusini sio tu kuna Kamati ya Mashirika ya Umma bali pia kuna Wizara inayosimamia Mashirika ya Umma (Ministry of Public Entreprises). Kimsingi Kamati ya POAC ilipaswa kuongezewa nguvu zaidi ili kufikia uwezekaji wa Serikali kwenye makampuni binafsi badala ya kuifuta. Uwezekaji wa Serikali kwenye makampuni kama BP, AirTel, Kilombero Sugar, SonGas nk hauna uangalizi wowote.
Uamuzi wa Spika wa Bunge kuifuta Kamati ya POAC ni uamuzi unaorudisha nyuma juhudi za nchi kujenga asasi za uwajibikaji, ni kinyume cha sheria ya ukaguzi wa umma inayotaja Kamati tatu za Bunge za kusimamia fedha za Umma na ni kinyume cha Katiba ya nchi. Spika wa Bunge anasema kazi za Kamati ya POAC zitafanywa na Kamati ya PAC; Tanzania ina jumla ya Mashirika ya Umma 258 yenye thamani ya shilingi trilioni 10.2 mpaka mwezi Juni mwaka 2012, hata kamati ya POAC ilikuwa haiwezi kushughulikia Mashirika yote ya Umma katika mwaka mmoja, PAC itawezaje kusimamia Wizara za Serikali, Mikoa na wakala za Serikali na wakati huo huo Mashirika ya Umma 258? Kwa vyovyote vile Taifa linarudi miaka ya kabla ya 2008 ambapo Mashirika ya Umma yalikuwa kichaka cha kuiba fedha za Umma. Hivi karibuni Kamati ya POAC iligundua mtindo wa Wizara za Serikali kupeleka fedha Serikali kwenye Mashirika na kutumia kifisadi ili kukwepa ukaguzi kwenye Wizara (Wizara ya Utalii ilipeleka zaidi ya shilingi 600 milioni Bodi ya Utalii mwaka 2010/2011). Ikumbukwe pia wizi wa EPA, MEREMETA na hata uuzaji holela wa baadhi ya mali za Serikali kupitia ubinafsishaji ulifanyika nyakati ambazo Bunge halina kamati inayosimamia Mashirika ya Umma.
Kwa vyovyote vile Spika wa Bunge amedhihirisha namna ambavyo anafanya maamuzi bila kuzingatia maslahi ya nchi wala kuzingatia historia ya uwajibikaji katika nchi. Namna mijadala ya Bunge inavyoendeshwa, namna anavyobeba ajenda za Serikali katika kujenga Bunge kibogoyo na namna anavyofanya maamuzi kwa kukurupuka, inahitaji hatua za kuokoa misingi ya uwajibikaji wa nchi. Ni lazima Spika wa Bunge adhibitiwe kwa kuondolewa katika nafasi hiyo haraka iwezekanavyo. Spika lazima ajue kwamba Mamlaka yapo kwa wananchi na yeye ni msimamizi tu wa vikao vya Baraza la wananchi liitwalo Bunge. Anna Makinda lazima adhibitiwe, vinginevyo nchi yetu itaumia.

 

 
Friday, 08 February 2013 14:15 Al News - Political Issues
Print PDF

Ndugai kamzima Mbatia? Dawa yake Katiba Mpya
Bunge ni muhimili muhimu sana. Wenyewe ndiyo unaotunga sheria na kuisimamia serikali. Kosa kubwa ambalo lipo kikatiba ndani ya nchi yetu kwa sasa ni kuacha mwanya wa viongozi wa muhimili huo kuwa na maslahi na vyama vinavyounda chombo hicho.
Mathalan, Spika wa Bunge anatoka chama kimoja, usimamizi wake kwenye chombo hicho lazima utakosolewa mara kwa mara hata kama atakuwa anatenda haki. Na pale atakapoonekana anakwenda kinyume na matakwa ya chama kilichomuweka pale, atakalia kuti kavu.
Spika wa Bunge, Anne Makinda ni mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ni mbunge, vilevile ameupata uspika kwa idhini ya chama hicho kinachotawala nchi kwa sasa. Swali je, anawezaje kukiuka matakwa ya CCM? Jibu ni kwamba hilo haliwezekani.


Spika wa Bunge la Tisa, Samuel Sitta, ilisemekana uongozi wake unakinzana na serikali ambayo inaongozwa na CCM. Matokeo yake, kuna kipindi ikaelezwa anatakiwa kutimuliwa ndani ya chama, baadaye imekuwa ngumu kurudi kwenye kiti hicho, akawa waziri.
Kama Sitta alishindwa kurudi kwenye kiti chake kwa sababu ya kuonekana hakipendelei chama chama chake, maana yake Makinda naye ataishi kwa angalizo hilo. Hatataka wabunge wa upinzani waiaibishe serikali ambayo inaongozwa na CCM.
Sura iliyopo sasa ni kwamba wapinzani hawana uhuru wa kuiwajibisha serikali ikiwa wabunge wengi ni kutoka CCM, spika wa bunge na wenyeviti wote ambao husimamia vikao vya bunge, wanatokea chama hicho. Hata kama watapewa uhuru, itaonekana ni sawa na mapenzi ya mama wa kambo.
Tukio la Ijumaa iliyopita, pale hoja ya Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia ambaye ni mwenyekiti wa NCCR Mageuzi kuhusu elimu, imenifanya niielekeze kalamu yangu kuandika kuhusu uhuru wa kibunge kama mhimili tunaoutaka baada ya katiba mpya.
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, kwa kutumia mamlaka ambayo anayo, aliiahirisha hoja hiyo kufuatia ombi la Mnadhimu Mkuu wa Serikali, William Lukuvi (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu na Bunge), aliyesimama kwa niaba ya serikali, kutaka hoja iahirishwe kwanza.
Mbatia alipingana na ombi hilo, matokeo yake Ndugai akauliza wanaoafiki na wasioafiki, majibu ya ndiyo na siyo yakasikika, naibu spika akasema waliosema ndiyo wameshinda. Wapinzani wakapingana na hilo, wakaomba muongozo, hawakusikilizwa.
Ndugai ni mwana CCM ambacho ndicho chama kinachoongoza serikali. Kwa uamuzi alioufanya ni wazi atatafsiriwa kama amemzima Mbatia na wabunge wengine wa upinzani ili kuiokoa serikali. Alichokifanya, kwa wapinzani, hakiwezi kuonekana ni uimara wake wa kusimamia sheria za kibunge, bali anasomeka ni mbabe.
Tafsiri wa wabunge wa upinzani kususia kikao cha bunge na kutoka nje ya ukumbi Ijumaa iliyopita, maana yake wanaionesha jamii ya Watanzania kwamba wanaonewa bungeni. Binafsi siwezi kumlaumu Ndugai, nailaumu katiba ambayo inaminya uhuru na demokrasia ndani ya bunge.
Ni usaliti na unafiki mkubwa kwa Ndugai kwenda kinyume na matakwa ya CCM wakati ndicho chama kinachomfanya aitwe naibu spika leo. Ndicho kilichompa ubunge, kadhalika anaishi kwa kutekeleza sera na ilani zake. CCM ikishindwa, madaraka aliyonayo hatapata.
Kama atabaki kuwa mbunge, maana yake atakuwa mpinzani. Badala ya kushiriki kuunda serikali, atakuwa mmoja wa wakosoaji. Hata kama siyo kushindwa kwa CCM, yanaweza kuibuka ‘majungu’ kama yale yaliyokuwa yanasemwa enzi za Sitta. Nani anataka?
Hoja ya Mbatia ilikuwa nzuri kweli, kwa maana hakuna mtu ambaye haelewi kwamba elimu yetu inakwenda arijojo. Sasa kitendo cha mawaziri (waziri na naibu wake), kushindwa kutekeleza walichoahidi kwenye kikao kilichopita, kupeleka mitala bungeni, ni kosa kubwa ambalo wabunge waliliona.
Mbaya zaidi, walifanya hivyo kipindi wanafahamu kwamba kuna hoja binafsi ya Mbatia kuhusu elimu. Waziri wa Elimu, Shukuru Kawambwa na naibu wake, Philipo Mulugo, pengine walisahau, walidharau au walifanya uzembe, sasa watawajibishwaje ikiwa hoja ilizimwa?
Twende tukajenge bunge la kidemokrasia, dawa ni moja tu, katiba mpya itamke kwamba spika, naibu wake na wenyeviti wote, wasiwe na vyama.

 

 
Sunday, 03 February 2013 12:09 Al News - Political Issues
Print PDF

Siasa na ukosefu wa wawakilishi makini ni chanzo cha machafuko Mtwara

Nimeshawahi kuandika makala huko nyuma, nikitanabahisha kwamba siasa zinaipeleka nchi pabaya. Tupo kwenye kipindi kigumu sana. Hatuoni misimamo ya kitaifa, kila jambo lazima ligawe wapinzani na serikali.

Nilishangazwa sana na jinsi ambavyo baadhi ya wapinzani walivyokuwa wanaunga mkono vurugu za kidini. Bila kutafuna maneno, ukweli uliopo sasa ni kwamba wapinzani wanalazimisha mitaji ya kisiasa kwenye machafuko.

Hata kama ni kweli Waislam wana madai ya msingi, kivipi usiwaunge mkono wakati mwafaka, ukangoja kipindi ambacho Makanisa yanachomwa moto ndipo utoe tamko la kuhalalisha harakati za akina Issa Ponda?

Ni wazi kwamba tamko hilo lilimaanisha Waislam waendelee na kile walichokuwa wanakifanya. Kauli hizo, zilitaka Wakristo nao waamke kujibu mashambulizi, baada ya hapo taifa liyumbishwe na vita ya kiimani.

Ni kweli kwamba serikali imeshindwa kufanyia kazi madai ya Waislam lakini anayekwamisha hayo siyo Makanisa. Wanasiasa wanajua athari, ila kwa sababu malengo yao ni mtaji wa kisiasa, wakaunga mkono ili vurugu ziendelee.

Gesi Mtwara ni sakata lenye umaarufu mkubwa nchini kwa sasa. Unapolitazama kwa kina, unaweza kuona makosa ya serikali, vilevile udhaifu wa kukosekana wawakilishi makini, mwisho siasa zimesababisha vurugu.

Haiwezekani mkoa ukawa na wabunge pamoja na maadiwani, hata siku moja hawajawahi kuwa na kauli nzito za kuishinikiza serikali dhidi ya madai ya gesi, matokeo yake wanaibuka wananchi, wanaandama, machafuko yanaibuka, vifo vinatokea..

Ile wananchi kuandamana wenyewe, maana yake kuna mambo mawili, moja linaweza kuwa sahihi. Mosi, wawakilishi na wananchi wana mitazamo tofauti, pili, wawakilishi wamelala, sasa wananchi wameamua wenyewe kusimama mstari wa mbele kudai kile wanachoamini ni haki yao.

Kama wawakilishi wanakubaliana na serikali, maana yake kuna tafsiri mbili, moja ndiyo ukweli. Mosi, wawakilishi wameshindwa kufanya kazi ya kuwaelimisha wananchi, pili, wawakilishi wamekubaliana na serikali kinyume na matakwa ya wananchi.

Kabla ya wananchi kuandamana, hatukuwahi hata mara moja kuona wabunge au misimamo ya madiwani katika Halmashauri za Mtwara, wakisimamisha mishipa kupinga gesi kusafirishwa kutoka mkoa huo.

Maana yake wananchi Mtwara wameamua kujisemea wenyewe, wamewaweka kando wawakilishi wao. Wamewaona maadui, kwa hiyo wakaamua kuwachomea moto nyumba zao. Ni aibu, mkuu mkoa, wabunge, wangejiuzulu ingefaa zaidi.

Vurugu za Mtwara, zitoe elimu kuwa Katiba Mpya inafaa kutamka kwamba wabunge hawapaswi kuwa mawaziri. Akina George Mkuchika na Hawa Ghasia inaonekana wanashindwa kufanya kazi ya uwakilishi ipasavyo, badala yake wanawajibika kwa serikali. Kosa kubwa.

Siasa; vyama vinaamini kuwa migogoro ya wananchi kama ilivyo Mtwara kwa sasa, kwao ni mtaji. Badala ya kujishughulisha kutoa elimu na kuwasaidia namna bora ya kudai haki bila machafuko, wao wanaunga mkono bila hata kuwapa tahadhari ya vurugu zao.

Serikali; bila shaka imeshajifunza wananchi wa Mtwara wanahitaji nini. Hivyo basi, inafaa kutumia busara za kidiplomasia kulimaliza hili jambo na amani irudi kwenye mkondo wake. Serikali inaposhindwa kuelewana na raia wake, hutoa picha kwamba inaongoza kiimla. Kwa Tanzania bado hatujafika huko.

Makala haya ni maoni ya mwandishi, siyo msimamo wa DeiwakaWorld.

 

Page 5 of 49

<< Start < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > End >>