Music | Lifestyle+Fashion | Antivirus | Love+Relationships | Business+Politics | Sport | TUMA Registrations

You are here:   HomeAll The News
| + -

News

Select a news topic from the list below, then select a news article to read.
Monday, 13 May 2013 00:00 Al Music
Print PDF

Ruge, Kusaga wakimbilia mahakamani, wamshatki Jide

Staa wa Bongo Fleva, Judith Wambura 'Lady Jaydee', leo alifika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, kufuatia kufunguliwa kesi ya madai katika mahakama hiyo.

Katika hati ya madai hayo, mwanamuziki huyo anashtakiwa na viongozi wa Clouds Media Group ambao ni Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga.

Tuhuma za kesi hiyo zinatarajiwa kusomwa mahakamani hapo na Hakimu, Athuman Nyamrani Mei 27 mwaka huu.

Jaydee aliwasili mahakamani hapo akiwa na mumewe, Gadner G. Habash, mishale ya saa 6 mchana na kuongoza moja kwa moja chumba cha makarani wa mahakama hiyo ambao aliwakabidhi hati ya mashitaka hayo.

Awali, ilielezwa kuwa Jide leo angefikishwa Mahakama ya Kinondoni, Dar bila kutajwa aina ya mashitaka yanayomkabili.

Taarifa za mwanadada huyo kufikishwa mahakamani hapo, ziliibuka chinichini kwenye mitandao ya kijamii, mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo baadaye Lady Jaydee alihoji kuwa pengine yeye ndiye anayestahili ‘kukinukisha’ kwa kuwapeleka mahakamani wasanii walio chini ya Tanzania House of Talent (THT), Estalina Sanga ‘Linah’ na Elias Barnaba.

Jide alisema kuwa aliwalipa Lina na Barnaba kianzio cha shoo yake ya Mei 31, mwaka huu kisha kumchomolea dakika za mwisho.

“Hivi mahakamani sitakiwi kwenda mimi ambaye wasanii wao wamechukua advance na kuafiki mbele ya camera na wakanipa, It wasn’t me?” aliandika Lady Jaydee katika mtandao wa Twitter.

KUMBUKUMBU

Kumbukumbu inaonesha, miongoni mwa maneno ambayo yanadaiwa kuwa yaliuchafua uongozi wa Clouds ni yale ambayo Lady Jaydee aliyaandika kupitia blogu yake hivi karibuni, akitoa waraka aliouita wosia kwa Rugen a Kusaga ikitokea yeye akitangulia kufa kabla yao.

Katika wosia huo, Jise alisema kuwa Rugen a Kusaga ni watu wabaya, wanaomuua kimuziki, akatamka kwamba siku akifa redio yao isipige nyimbo zake wala kutoa ripoti yoyote ya msiba, wao wenyewe wasisogee kumzika na watu wakitokea, watakaokuwepo wawapige mawe.

RUGE HAKUKAA KIMYA

Hata hivyo, siku chache baada ya Lady Jaydee kuandika wosia huo mzito, Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba alitumia Kipindi cha Power Breakfast kuzipangua hoja moja baada ya nyingine na mwishoni kumalizia kwa kusema Jide anapaswa kusoma alama za nyakati kwani umri unakwenda na muziki anapaswa kujipanga vizuri ili uweze kujimudu pindi zamu ya kushuka kwenye gemu inapofika.

Kuhusu wito wa mahakamani, Jide ‘ali-tweet’: “Nimepata taarifa zisizo rasmi kuwa nimefunguliwa kesi mahakamani, natumaini sitaitwa kizimbani tar. 31 May ambayo ndiyo siku ya show.”

Baadaye aliongeza: “Ratiba ya usiku wa leo (Ijumaa iliyopita) ni Machozi Band kama kawaida, ila ratiba ya Jumatatu (leo) natakiwa Mahakama ya Kinondoni. Taarifa zaidi zitafuata nikijua kinachoendelea. Ila kwa leo mje tuburudike Nyumbani Lounge mpaka asubuhi.”

 
Wednesday, 08 May 2013 03:41 Al Political Issues
Print PDF

Ukweli kamili kuhusu bomu lililotupwa kanisani Arusha

Kama tulikuwa tunasubiri dalili kubwa zaidi zijitokeze ndipo tutambue kwamba hali ya nchi inatisha, tukio la bomu kutupwa kanisani, likasababisha vifo na majeruhi, lipimwe kama ishara ya juu kabisa.

Pamoja na kila kinachosemwa kuzunguka tukio hilo, ukweli ni kwamba serikali ina kazi kubwa ya kufanya kutuliza mdudu hatari wa ubaguzi ambaye anaelekea kufanikiwa kuwagawa Watanzania kutokana na matukio ya aina hiyo.

Kudhihirisha hali ilivyo mbaya, maneno ya chuki ya kidini yalitawala jijini Arusha na katika mitandao ya kijamii kuzunguka nchi nzima, baadhi ya wakosoaji wakiwashutumu watu wa dini fulani kuhusika.

NI UGAIDI TU

Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit, Arusha, lililipuliwa na bomu la mkono, Jumapili iliyopita, saa 4:30 asubuhi.

Iliripotiwa juzi (Jumapili) kuwa mmoja wa watuhumiwa wa tukio hilo, anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, mtu huyo alikamatwa muda mfupi baada ya msako dhidi ya washukiwa kuanza.

Kuhusu chanzo au sababu ya wahusika kufanya ulipuaji huo, bado ni siri nzito lakini Watanzania wameshauriwa kuwa watulivu, kwani hilo ni moja ya matukio ya kigaidi ambayo yanapenyezwa nchini kwa sasa.

“Sisi Watanzania tunajuana, hakuna Muislamu anayeweza kufanya shambulio dhidi ya Wakristo, kadhalika hakuna Mkristo anayeweza kufanya shambulio dhidi ya Waislamu, walipuaji ni magaidi, wakamatwe na washtakiwe kama magaidi.

“Haya maneno ya kusema watu wa dini moja wamewashambulia wa dini nyingine ni uchochezi mbaya na maneno ya aina hiyo yakiendelea yatatugawa Watanzania,” alisema Aminieli Moba, juzi, akiwa eneo la tukio, muda mfupi baada ya mlipuko.

Maneno ya Moba, hayapishani na ya Tito Hebrew, aliyeandika kwenye ukurasa wake wa Facebook: “Jamani hakuna udini, kuna chokochoko nyingi zinaibuliwa hapa. Watu walishataka kutugombanisha kwa njia za kisiasa wakashindwa.

“Kuna kipindi walijitahidi kutugombanisha kwa misingi ya ukabila ikawa ngumu, sasa hivi wanaamua kutumia njia za udini. Watanzania tunatakiwa tuutegue huu mtego, vinginevyo tutaingia kwenye vita ya sisi kwa sisi.”

TUKIO LENYEWE

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, akiwemo mtoto mdogo (wote tunawahifadhi), mwanaume aliyevalia koti kubwa lenye kofia, akiwa amejifunika usoni, alitokea upande wa kushoto wa kanisa hilo kwa mbele na kutupa bomu hilo.

“Nilikuwa nimesimama ghorofani, nikamwona mtu akiwa na koti la mvua akisogea mbele ya kanisa na kurusha kitu kilichotoa mlio mkubwa na baadaye watu walianza kulia kwa sauti ndiyo nikajua lilikuwa ni bomu,” alisema shuhuda mmoja.

Shuhuda mwingine alisema: “Yule mlipuaji alikuwa na mwenzake na walifika pale kanisani wakiwa na gari. Baada ya kurusha bomu, alirudi kwenye gari kisha wakakimbia.”

Hata hivyo, shuhuda huyo ambaye ni mtoto mdogo, hakuweza kufafanua gari hilo ni aina gani wala namba zake za usajili.

VIFO

Kwa mujibu taarifa za vifo mpaka sasa, watu watatu wamesharipotiwa kufariki dunia kutokana na tukio hilo.

Watu 70 walijeruhiwa katika shambulio hilo na wote walifikishwa kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru.

Waliojeruhiwa katika tukio hilo, wengi wao walionekana wakivuja damu nyingi, zilizolowanisha kabisa nguo zao.

Wengi wa waliojeruhiwa, walikatika viungo na wengine wamechanwachanwa, hivyo kuacha taharuki isiyomithilika.

MWAKILISHI WA PAPA CHUPUCHUPU

Mwakilishi wa Papa Francis I hapa nchini, Balozi Francisco Padilla, alinusurika kifo katika shambulio hilo.

Balozi Padilla aliyekuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa kanisa hilo, alikoswa na bomu, kwani lililipuliwa wakati akikamilisha ratiba za kubariki kanisa kabla ya kukata utepe, kuashiria mwanzo wa utoaji wa huduma za kikanisa.

Kanisa hilo ni jipya na ujenzi wake ulikamilika hivi karibuni, hivyo kugeuka gumzo kutokana, likitajwa kuwa moja ya makanisa yaliyojengwa kisasa kabisa ukanda wa Afrika Mashariki.

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Arusha, Josephat Lebulu, pamoja na  mapadri zaidi ya 200, walihudhuria hafla hiyo ya uzinduzi wa kanisa hilo lakini wote wamenusurika.

NI MAAFA KATIKATI YA SHEREHE

Msemaji wa Kanisa Katoliki Parokia ya Olasit, Father Festus Mwangwangi, alisema kuwa sherehe za uzinduzi zilianza vizuri lakini mambo yaliharibika baadaye.

Alisema, kabla ya tukio hilo waumini wa kanisa hilo walianza maandamano kuanzia Kanisa Katoliki la Burka ambalo ni kanisa mama, wakiongozwa na Askofu Lebulu, na ilipofika saa 3.30 asubuhi, walifika katika kanisa hilo la Mtakatifu Joseph.

“Maandamano yalipokamilika, balozi wa Vatican (mwakilishi wa Papa), aliwasili katika msafara wake na mwenyeji wake ambaye ni Askofu Lebulu, kisha akamtembeza kulikagua kanisa hilo.

“Baada ya kulikagua kanisa, lilifuata tendo la kubariki maji ambayo yangechanganywa na chumvi kisha kutumika kulibariki kanisa lakini tukiwa kwenye hatua ya kubariki maji ndipo mlipuko mkubwa ulisikika,” alisema Father Mwangwangi.

UVUMI KUHUSU SIASA

Kwa upande mwingine, yapo madai yaliyopo mkoani Arusha kwamba bomu hilo pengine ni njama za wanasiasa.

Inadaiwa kuwa kuelekea uzinduzi wa kanisa hilo, kuna mmoja wa mawaziri wakuu wastaafu, alitajwa sana kuwa angekuwa mgeni rasmi.

“Pengine watu wabaya dhidi ya huyo mheshimiwa, waliamini huo uvumi, sasa wakaona hiyo ndiyo sehemu ya kutekeleza njama zao,” alisema mkazi mmoja wa Arusha, Philipo Abdiel.

LEMA AKOSOLEWA

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, alifika eneo la tukio muda mfupi baada ya bomu kulipuka na kutoa matamshi makali dhidi ya serikali na udini.

Hata hivyo, wananchi wa Arusha waliozungumza na ripota wetu, walisema kuwa wanamheshimu sana Lema na wanampenda kama mbunge wao lakini anakosea kuweka siasa katika tukio zito kama hilo la ugaidi.

“Kuna mambo akichanganya na siasa itakuwa sawa lakini siyo hili. Lema anatakiwa kushirikiana na serikali katika vita dhidi ya ugaidi ambao unapenyezwa nchini,” alisema Rosemina Kiwia, mkazi wa Ngarenaro, Arusha.

POLISI WANENA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alisema: “Uchunguzi makini utafanyika. Hapa tutawaleta wataalamu wa mabomu na baada ya uchunguzi ndipo tutatoa taarifa rasmi ya jeshi la polisi.”

MKUU WA MKOA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati vyombo vya dola vikiendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

“Polisi kutoka makao makuu ya jeshi pamoja na wataalamu wa mabomu kutoka makao makuu wanatarajiwa kufika katika eneo la tukio ili kuongeza nguvu,” alisema Mulongo.

KAULI KALI YA WAZIRI NCHIMBI

Jana, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, alisema kuwa watu wanaoeneza chuki za kidini hawatavumiliwa, watachukuliwa hatua kali sana.

“Tunaendelea na uchunguzi wetu lakini kuanzia sasa, serikali haitawavumilia watu wanaoeneza chuki za kidini, tutawachukulia hatua kali ili iwe fundisho,” alisema Nchimbi.

JK ASITISHA SAFARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete, alikuwa kwenye ndege safarini kwenda Kuwait, wakati shambulio hilo la bomu lilipofanyika na lakini alipofika na kujulishwa kilichotokea, alisitisha ziara yake na kurudi nchini.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, alisema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo, aliwasiliana na viongozi mbalimbali nchini kwa ajili ya kupata picha halisi ya tukio.

“Sasa hivi (jana mchana), yupo njiani, atafika Dar es Salaam halafu kesho (leo) asubuhi atakwenda Arusha,” alisema Rweyemamu.

WALIOKAMATWA

Mpaka sasa, watu wanane walishakamatwa, mmojawapo akiwa mtuhumiwa nambari moja, anayefahamika kwa jina la Victor Ambrose, 20.

Inaelezwa kuwa Ambrose, aliwataja wenzake watatu ambao nao walikamatwa.

Vilevile, raia wanne wa Saudi Arabia, walikamatwasiku ya tukio wakiwa safarini kuelekea Kenya, wakipitia mpaka wa Namanga.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ametoa taarifa bungeni leo kuwa raia wa Saudi Arabia, waliokamatwa ni kwa ajili ya upelelezi kama kweli wanaweza kuwa wanahusika au la!

“Mpaka kesho, itakuwa imeshajulikana kama kweli wale wanahusika au la,” alisema Pinda.

 

 
Friday, 03 May 2013 07:49 Al Love+Relationships
Print PDF

Aunt Ezekiel, mumewe wakutana Sauzi

Mwigizaji Aunt Ezekiel ameonekana Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, akikwea pipa kumfuata mumewe, Dimonte Almousa, pande za Afrika Kusini.

Ripota wetu alimshuhudia staa huyo akikwea pipa mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya mumewe aishiye Dubai kumpa taarifa kwamba atakuwa Afrika Kusini kikazi hivyo wakutane kwa muda.

“Nakwenda Sauzi kwa muda wa wiki moja kwa ajili ya kukutana na mume wangu, sitakaa sana nitarudi Bongo kisha nitajiandaa kumfuata nyumbani kwetu Dubai,” alisema Aunt.

Hivi karibuni Aunt aliweka bayana kuwa hata iweje, kamwe hawezi kutengana na mumewe huyo.

 
Friday, 03 May 2013 07:27 Al Music
Print PDF

Mashambulizi ya Jaydee kwa Ruge, Kusaga yaibua msukosuko

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ ameendelea kuwakaba koo wakurugenzi wa Redio Clouds FM, Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba.

Jide, ameibua msukosuko wa aina yake nchini kufuatia tamko lake alilotoa jana, akibainisha kwamba Kusaga na Ruge si watu wema na hata akifa, redio yao isitangaze kifo chake wala kupiga nyimbo zake, vilevile na wao hawatakiwi kuhudhuria.

Hili ndiyo tamko lenyewe…

WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA

Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi na bado naendelea ku-experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.

Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao. Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.

Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu. Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.

Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa. Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.

Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.

Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu. Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige mawa enyi mtakaokuwa hai baada yangu.

Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu. Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.

Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.

Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka. Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia..

Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..

Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie? Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.

Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili. Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.

Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani? Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi? Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.

Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.

Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma? Roho gani hiyo??

Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu

 

 
Friday, 03 May 2013 06:21 Al Lifestyle+Fashion
Print PDF

Mbwa ndiye faraja pekee ya Wema kwa sasa

Miss Tanzania 2006-2007, Wema Sepetu amefunguka kuwa hakuna kitu kinachompa faraja kubwa kwa sasa kama mbwa wake, Ivan na Gucci.

Wema alisema hawezi kukaa zaidi ya siku tatu bila kuwaona mbwa wake hao kwani amewazoea kwa kuwa humuondolea ‘stress’ za hapa na pale.

“Juzikati nilikwenda Arusha mara moja tu siku hiyohiyo nikawa nawakumbuka Ivan na Gucci mpaka nikawa natamani kurudi kwa ajili yao, kusema kweli hawa ndiyo kila kitu kwangu,” alisema Wema na kuongeza:

“Nimewazoea lakini wao pia ndiyo zaidi, hawataki kubanduka pindi ninaporudi kutoka katika kazi zangu, mtu akiwachukua tu umewakorofisha.”

 
Friday, 03 May 2013 05:47 Al Lifestyle+Fashion
Print PDF

Mastaa wa Bongo, pete nyingi ndoa sifuri

Katika ulimwengu huu kuna mambo mengi yanayofurahisha. Yapo pia yanayosikitisha na utapeli katika uhusiano wa kimapenzi umetamalaki.

Utangulizi huo una maana kuwa katika jamii inayotuzunguka inabidi mtu uwe makini la ivyo utajikuta kwenye wakati mgumu hasa kwa wasichana wanaohitaji kuolewa.

Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanaume kuwarubuni wanawake wakiwadanganya kuwa watawaoa, ahadi ambazo hazitimii kwani mapenzi yao huwa yanaishia njiani kabla hawajatimiza lengo na kuwaacha wenzao katika maumivu makali.

Katika ulimwengu wa mastaa wa Kibongo, ishu hiyo ndipo nyumbani kwao ambapo leo katika makala haya tutaona orodha ya wasanii ambao wamevishwa pete za uchumba lakini suala la ndoa limeishia ndotoni.

Ni kama wanaota lakini wakiamka hujikuta wakijuta kuwa walikosea wapi. Kinachoonekana kwa sasa ni kwamba pete ya uchumba ni ndoano ya kumnasa mwanamke na baada ya kukidhi matwakwa humwacha bila kutimiza ahadi ya ndoa.

FLORA FESTO MVUNGI

Ni mwigizaji wa filamu za Kibongo anayeishi kinyumba na mwanamuzki wa Kizazi Kipya, Hamis Ramadhan Baba ‘H. Baba’.

Tangu Flora avishwe pete ya uchumba na H. Baba pamoja na kutolewa mahari, siku zimesonga bila kuona suala la ndoa likiendelea.

Wasanii hawa kila wakiulizwa kuhusu suala la ndoa huwa wanajibu hivi karibuni ambapo kwa sasa kuna madai kuwa tayari Flora ana ‘kibendi’.

ROSE DONATUS NDAUKA

Ni staa mkubwa wa filamu za Kibongo ambaye alichumbiwa kwa muda mrefu na jamaa aliyekuwa mmoja wa kundi la kitambo la Bongo Fleva kutoka Tanga la TNG, Malick Bandawe.

Rose amekuwa akiahidi kila kukicha kuwa harusi yake iko mbioni lakini umepita muda mrefu hakuna ndoa wala nini na badala yake wamebaki kuishi pamoja kama mume na mke.

OTILIA BONIFACE

Ni mkata mayenu kiraka wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo Staili’. Alivishwa pete ya uchumba miaka miwili iliyopita na mume wa mtu anayejulikana kwa jina moja la Ally lakini mpaka sasa ndoa imebaki ndotoni.

Otilia na mchumba wake huyo wanaishi pamoja kama mume na mke na suala la ndoa bado wanajiandaa.

SUZAN CHUBWA ‘QUEEN SUZY’

Ni mnenguaji bei mbaya wa Bendi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’. Alivishwa pete ya uchumba zaidi ya miaka miwili iliyopita na aliyekuwa rapa wa bendi hiyo, Aimerichard Mwamba ‘G-Seven’ ambaye kwa sasa amehamishia makazi yake Nairobi, Kenya na kumwacha Suzy Bongo.

G-Seven alimposa Suzy pamoja na kumvisha pete ambapo uchumba wao ulidumu kwa muda mrefu kabla ya hivi karibuni bishosti huyo kuweka wazi kuwa ameamua kuachana naye kwa sababu aligundua kuwa siyo mwaminifu.

ISABELA MPANDA

Ni Miss Ruvuma 2006. Anasaka mkate wa siku kupitia filamu na muziki wa Bongo Fleva. Alivishwa pete ya uchumba kitambo na kutolewa mahari na mwanaume jina kapuni lakini aliishia kupewa mimba na kuzaa.

Baada ya kuzaa Isabela mpaka sasa hajaolewa na amejaliwa kuwa na watoto wawili kila mmoja na baba yake huku ikifahamika kuwa yupo kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki Luteni Kalama.

MIRIAMU GERALD

Ni Miss Tanzania 2009 aliyevishwa pete ya uchumba na msanii wa filamu za Kibongo, Kennedy Victor ‘Kenny’. Walipanga kufunga pingu za maisha mwezi Juni, mwaka jana lakini hadi unaposoma hapa hakuna chochote zaidi kujaliwa mtoto mmoja wa kiume.

WEMA SEPETU

Ni mwanadada mrembo kutoka kiwanda cha filamu za Kibongo. alivishwa pete ya uchumba na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond Platnumz’ lakini mapenzi yao hayakufika mbali, waliishia kuachana na mambo ya ndoa yakaishia hapo huku bidada akiendelea kujikusanyia pete za uchumba kabatini kwake baada ya ile ya Yusuf Jumbe.

SHAMSA FORD

Ni staa wa filamu za Kibongo ambaye kwa muda mrefu amechumbiwa na jamaa mmoja aitwaye Dick. Uchumba wao una zaidi ya miaka miwili lakini ndoa imekuwa ni kitendawili huku wakijaliwa mtoto mmoja wa kiume aitwaye Terry.

SALMA JABU ‘NISHA’

Ni staa wa filamu za Kibongo ambaye aliwahi kudaiwa kuvishwa pete ya uchumba na mwigizaji mwenzake aitwaye Godfrey Kusila kabla ya uchumba kuvunjika na penzi kuhamia kwa mwanamuziki Elibariki Emmanuel ‘Ney wa Mitego’. Hata hivyo, kwa Ney wa Mitego napo uchumba uliota mbawa pamoja na kuwa na mbwembwe nyingi.

 
Friday, 03 May 2013 05:28 Al Political Issues
Print PDF

Nani fisadi yupi siyo, Usalama wa Taifa wakiamka nchi itanyooka

Idara ya Usalama wa Taifa ni nyeti. Hali ya ufisadi ilivyofikia sasa hivi, haiwezi kumalizwa na wanasiasa peke yao. Programu ya dharura inapaswa kuchukua nafasi na watekelezaji wake wanatakiwa wawe wazalendo kweli. Wenye tamaa wakae mbali, maana ndiyo wametufikisha hapa.

Pamoja na uwepo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Usalama wa Taifa wanaweza kuwa msingi wa vita dhidi ya ufisadi. Kama wamelala katika eneo hili, wanapaswa kuamshwa, watambue kwamba maisha ya Watanzania yanahitaji nguvu na maarifa yao.

Watumishi wengi wa umma wanaishi maisha ya bandia. Wanafanya mambo makubwa tofauti kabisa na mishahara pamoja na marupurupu yao. Wanajenga majengo ya kutisha na kuendesha magari ya kufuru. Ajabu ni kwamba watu hao hawaguswi. Usalama wa Taifa mpo wapi?

Kama aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, aliandamwa kwa kununua nyumba ya shilingi milioni 650, ni kwa nini maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, hawafuatiliwi na hawachunguzwi? Kwa maana wanayoyafanya ni mazito.

Akaunti yake ina mabilioni ya shilingi, amezipataje? Amejenga nyumba yenye thamani ya shilingi bilioni tatu, amepata wapi fedha za kufanya hivyo? Anamiliki magari ya kifahari, ukijumlisha idadi yake na kuyapigia hesabu, yanaweza kugharimu zaidi ya shilingi bilioni moja.

Anatembea na wapambe siyo chini ya 10, anakutana nao kwenye hoteli zenye hadhi ya nyota tano, anawanunulia chakula, wanakula mpaka wanasaza, anawanywesha pombe hadi wanalewa tilalila. Kwa siku moja anaweza kutumia shilingi 2,000,000, kwa siku 10, milioni 20 zinakatika.

Mshahara wake na marupurupu vimekaaje? Maana pamoja na matumizi hayo, anawalipia kodi za nyumba wapambe ambao kazi yao kubwa ni kumtafutia tu wanawake. Hawana kazi, kwa hiyo anawapa mpaka fedha za matumizi ya kuendesha familia zao na starehe ndogondogo.

Hao wanawake, wenye bahati wanajengewa nyumba, wapo wanaonunuliwa zikiwa zimekamilika. Wengine wanapangiwa, vilevile kuna wanaoishia kupewa fedha. Kuhonga magari ndiyo usiseme, utadhani anayatengeneza yeye. Turudi kwenye swali la msingi, anapata wapi pesa?

Ofisa wa TRA, hata akiwa kamishna hana ubavu wa kufanya vurugu hizo. Lazima tu atakuwa anaiba. Wizi wenyewe ni uhuni wa ulipaji kodi. Wanakula na wakwepaji, na kwa sababu fedha zinakuwa za haramu, haoni hata woga wa kuzichezea, ndiyo maana anazitumia kama fimbo.

Tunawaona, wakali wa vita za kugombea wanawake. Wanashindana kuhonga vitu vya thamani ili kupata mapenzi (ngono). Siku zote mwizi akili yake huwa inalala, ukomo wa mawazo yake huishia katika kuiba na kutumia. Anaiba nyingi, anafanyaje sasa? Hii ndiyo sababu ya kufanya vurugu nyingi mitaani.

Nidhamu ya utumishi wa umma ni jambo ambalo linapaswa kusukwa upya. Wengi wanajiangalia wao peke yao. Usalama wa Taifa wakiamua, wanaweza kuchunguza aina ya watu ambao wanafaa kuwatumikia wananchi. Wezi, wenye tamaa, watapanya pesa hawatakiwi.

Inashindikana nini kwa Usalama wa Taifa kuchunguza mishahara ya watumishi wa umma lafu wakaoanisha na matumizi yao, kujua nani fisadi yupi siyo? Ni hesabu ndogo, tena ni kazi ambayo haihitaji hata siku 30. Wakifuatiliwa, ndani ya wiki moja watakuwa wameshabainika.

Inawezekana Usalama wa Taifa wanafuatilia mambo mengi kwa ajili ya kuhakikisha nchi ipo salama, hili la ufisadi katika kipengele cha mapato ya watumishi wa umma dhidi ya matumizi, wanawaachia Takukuru. Hapo ndipo wanapofanya makosa makubwa.

Takukuru wanafanya kazi kwa mtindo wa mazoea. Pale walipo, hawashughuliki na mtu mpaka wapewe taarifa kwamba mhusika amepokea au yupo kwenye harakati za kula/kutoa rushwa. Akifuatiliwa bila taarifa, hiyo ni janja ya maofisa fulani na wakishapozwa hunyamazwa kimya.

Tunataka watu wanaothubutu. Wale watakaosimama leo na kusema ufisadi ufike mwisho. Wenye uchungu na jasho la walalahoi. Walio na nia thabiti ya kumkomboa Mtanzania na hili janga la ugumu wa maisha. Usalala wa Taifa amkeni leo, tuanze mapambano ya mapato dhidi ya matumizi kwa watumishi wa umma, tutawanasa mafisadi wengi sana.

 
Wednesday, 24 April 2013 19:47 Al Music
Print PDF

Jina la Biggie latumika kunadi mjengo

Mjengo wa kifahari uliopo eneo la Clinton Hill, Brooklyn, New York, Marekani, unauzwa kwa thamani ya dola za 750,000, sawa na shilingi 1.2.

Mchawi wa Freestyle, Christopher Wallace ‘Notorious B.I.G’, aliishi kwenye mjengo huo wakati akiwa mdogo.

Kwa vile B.I.G a.k.a Biggie aliishi hapo enzi hizo, wamiliki wa jengo hilo, wameamua kutumia jina lake kwa ajili ya kulinadi, kwa imani kwamba litapata wateja kwa urahisi.

Matangazo mengi mtandaoni, yanasomeka: “Nyumba aliyoishi Biggie inauzwa.”

Familia ya Biggie ambaye alifariki dunia miaka 16 iliyopita, haijatoa tamko kama inaona sawa au kuchukizwa na matumizi ya jina la mkali huyo wa Hip Hop katika mauzo ya mnada wa jengo hilo.

 
Wednesday, 24 April 2013 19:39 Al Sports News
Print PDF

Barthez njiapanda Taifa Stars

KOCHA Mkuu Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza kikosi cha pili cha timu ya taifa, Taifa Stars, ambacho atakitumia kuangalia wachezaji anaoweza kuwaita kwenye kikosi cha kwanza huku jina la kipa wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’ likiwemo na mchezaji kutoka England.

Akizungumza kabla ya kutaja kikosi hicho jana, Kim alisema hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4, 2013.

Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes, lakini hawajapata nafasi ya kucheza Taifa Stars.

“Leo (jana) ninatangaza timu ya pili ya Stars ambayo inaundwa na wachezaji wengi vijana wa umri chini ya miaka 20 na wachache ambao hawajapata nafasi ya kuichezea ile ya kikosi cha kwanza.

“Tofauti na vijana hao, pia nimeita wakongwe kama Barthez, Barnabas (Vicent) na David Mwantika kwa ajili ya kuwaangalia uwezo wao zaidi na kama nikiona wanafaa nitawapandisha kwenye timu ya kwanza,” alisema Kim.

Wachezaji walioitwa wataingia kambini Mei 2 hadi 6, mwaka huu. Walioitwa ni; Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) ambao ni makipa. Mabeki ni Kessy Hassan (Mtibwa Sugar), Kennan Ngoma (Barnsley FC, Uingereza), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), David Mwantika (Azam), Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Kagera Sugar), Waziri Salum (Azam), Samih Nuhu (Azam) na Emily Mgeta (Simba).

Viungo ni; Haruna Chanongo, William Lucian, Jonas Mkude, Edward Christopher, Abdallah Seseme, Ramadhan Singano (wote Simba), Mudathiri Yahya (Azam), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Jimmy Shoji (JKT Ruvu), Farid Mussa (Azam) na Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni; Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Jerome Lambele (Ashanti United), Zahoro Pazi (JKT Ruvu), Twaha Hussein (Coastal Union), Abdallah Karihe (Azam) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar) na Barthez.

 
Wednesday, 24 April 2013 19:19 Al Lifestyle+Fashion
Print PDF

Miss Utalii sasa kimeeleweka

Baada ya Kambi ya Miss Utalii Tanzania 2012/13 ambayo imeanza upya kwa kasi ya ajabu ambapo wadau mbali mbali ikiwa ni asasi za Serikali, Taasisi mbalimbali, Makampuni pamoja na watu mbalimbali wamejitokeza kudhamini Fainali Hizo za Miss Utalii Tanzania Taifa Ambazo zitafanyika Mwanzoni mwa Mwezi Ujao.

Walio jitokeza Kudhamini ni pamoja na. TANAPA, Ngorongoro Crater, Tanzania Tourist Board, Mtwana Catering, Ikondolelo Lodge Hotel, Sahara Media Group, Mbasha Entertainment, Sophia Records,Nyinda Hotel, Tanga Beach Resort, Retco, Tanzania School of Journalism and Mass Communication,  Oriental Berau De Change, Clouds Media Group, Times FM, Global Publishers, Tone Multimedia Group, Dar es salaam City College, Eden Hill College, Maweni Hotel.

Bado kuna wadau wengine mbalimbali ambao wanaendelea kujitokeza kwa ajili ya Kudhamini Fainali Hizo za Miss Utalii Tanzania 2012/13.

Mpaka sasa Kambi mpya ya Miss Utalii Tanzania 2012/13 ipo na inaendelea Vizuri, Warembo zaidi ya 30 wamejiandaa vizuri  kwa ajili ya Fainali Hizo zitakazo fanyika Mwanzoni mwa mwezi Ujao ikiwa ni pamoja na Kutoka Mikoa yote Tanzania, Kanda Maalum ya Zanzibar na Vyuo vikuu Tanzania.

Washindi wa 1-5 wa Fainali za Taifa ,watawakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya Dunia yakiwemo ya International Miss Tourism World, Miss Tourism United Nation, Miss Heritage World, Miss Tourism University World, Miss Globe International n.k

Miss Utalii Tanzania ,hadi sasa tunashikilia Jumla ya mataji 5 ya Dunia na kimataifa, yakiwemo ya Miss Tourism World 2005-Africa,Miss Tourism World 2006-SADC,Miss Tourism World 2007-Africa, Miss Tourism Model Of The World 2008-Personality n.k

 
Wednesday, 24 April 2013 19:07 Al Love+Relationships
Print PDF

Mrembo adai kuambukiza Ukimwi wanaume 1500

Simulizi yake ni hii;

Nilizaliwa mkoa wa Dodoma na nilishi vizuri tu tangu utotoni na hata sikujihusisha na ngono hadi nilipomaliza form 4 mwaka 2006 baada ya kumaliza nilikuja hapa Dar kuishi kwa mama mdogo aliyeolewa hapa Mwenge.

Nilipata marafiki wengi tu na kuna kijana mmoja alinitongoza kwa muda mrefu sana na siunajua vijana wengi hutumia muda mrefu kutongoza ili msichana unadhani kwamba labda huyo anakupenda kumbe anataka tu ngono na wadada wengi sana hudhani kufuatiliwa kwa muda mrefu na mvulana basi huyo yuko serious kumbe hakuna lolote.

Nilimkubalia tukawa wapenzi ila nilikataa kuhusu kufanya mapenzi maana anayekupenda kiukweli sio uongo lazima asitake ngono kabla ya ndoa.

Kwa miezi kama 5 hadi 6 aliniambia kuhusu kufanya mapenzi nilikataa alitumia mbinu nyingi sana kwa kunibembeleza na hata kulia mbele yangu ili tufanye tu mara moja ila nilikataa, alisema atavumilia hadi siku ya ndoa yetu ambapo tulipanga kuoana mwaka sept 2009.

Siku moja aliniambia twende kwenye kumbi za starehe na mimi kwa sababu ya upagani na kumwamini pia kwa sababu nampenda nilikubali tulienda huko na kulikua na bendi fulani maarufu ya mziki wa dansi ilikua inatumbuiza.

Tulitafuta sehemu na kukaa na mpenzi wangu akaagiza pombe alianza kunywa huku akinionjesha, nilikataa kwa sababu nilikua sijawahi kunywa pombe katika maisha yangu yote, hata sijui alinishawishi vipi nilijikuta nakunywa kidogo kidogo na kwa kuwa tulikaa pale kwa muda zaidi ya masaa 5 nadhani nikunywa kama bia 3 au 4 japokua nilikua nakunywa kidogo kidogo tu tena kwa kunywesha na mpenzi wangu maana nikama nikua nanyweshwa kila baada kama ya dakika 25 ndipo nakunywa mara moja na sikujuia kama nakunywa pombe ila niliihisi tu naonja ili kumlizisha mpenzi wangu.

Ilipofika saa 10 alfajiri nilihisi usingizi na pia nilijiona wa tofauti najua nililewa hata kama sikujua kama nimelewa maana nakumbuka tulitoka pale huku amenishika mkono huyo mpenzi wangu. Tulikodo tax na kuondoka na siku hiyo aliniambia twende kwake alikokua amepanga chumba maana tulikua na usingizi sana nilikubali huku nikidhani hatuwezi kufanya mapenzi.

Tulifika salama na kuingia ndani ukweli pombe ni kichocheo cha ngono na ningekua mimi ndio Raisi wa Tanzania ningefunga bar zote. Nilijikuta natamani kufanya mapenzi na huyu mpenzi wangu hata alikua hana nia maana alijua atanichukiza sana na uhusiano ungekufa siku hiyo lakini kwa sababu ya pombe nilimwambia siku hiyo tufanye kidogo maana mwili wangu unataka.

Ni kweli siku hiyo kwa sababu ya pombe nilifanya mapenzi na huyo mpenzi wangu na baadae akanipeleka nyumbani baada ya wiki mbili maana tulikaa wiki mbili bila kuonana alikuja na kunieleza habari ambayo sikuihitaji katika maisha yangu maana nilikua nasikia tu kwa watu wengine lakini sio kwangu alisema ”JANE ISHI KWA MATUMAINI KUANZIA SASA”

Nilidhani utani lakini aliniambia kuwa yeye ana UKIMWI tangu miaka mitano iliyopita na anapenda tu ngono maana hawezi kuacha.

Nililia sana na baada ya wiki moja baadae nikaenda kupima na kukutwa nina ugojwa ambao niliusikia tu kwa watu na chanzo cha yote ni pombe, kupenda starehe,disko na upagani unaotusumbua wanadamu wengi.

Nilikua na UKIMWI na kwa hasira maana mpenzi wangu alihamia Arusha huku akisema neno moja la mwisho kwamba ”shetani amemtuma kuwaambukiza wanadamu UKIMWI”

Sikujua, sikujua, sikujua, sikujuaaaaaaaaa, basi tu ooh YESU nihurumie mimi leo.Nilibebeshwa mzigo ambao haukunistahili mimi. Hata leo hua najiuliza kwamba nilijitunza kwa miaka 23 yote lakini pombe na huyu wakala wa shetani wamenifanyia hivi. Baada ya kujua nina UKIMWI na hali hiyo nikaikubali na kulikua na kundi kubwa sana la wanaume ambao walikua wamewahi kunitongoja na niliwakataa sana kwa sababu hii niliwakubali ili nami nife na wengi.

Nilianza kumkubali kila mmoja na kuna baba mmoja ambaye ana wake 3 niliwahi kumtukana sana kipindi cha nyuma kila aliponitongoza lakini wakati huu nilimkubali na hakuamini na tukafanya ngono tena bila kinga na akaniaachia pesa laki 6 kama zawadi ya kumkubali kumbe naye hakujua kuwa namwambukiza na hata leo hua nawahurumia tu wale wake zake ambao wana UKIMWI uliotoka kwangu.

Kiukweli tangu may 2009 hadi 2012 nimeshatembea na wanaume zaidi 1500 maana ilifika kipindi nala na wanaume 3 kwa siku na lengo langu niwakomeshe kama mimi nilivyokomeshwa na nina uhakika kutokana na mimi wameambukizwa UKIMWI wanadamu zaidi ya 10,000 na hili tangazo la ”TUKO WANGAPI” huwa linaniliza kila siku maana hata mimi najua kabisa nilianzisha mtandao kama huo wa ngono kwa idadi kubwa sana ya watu.

Nimeokoka miezi 7 iliyopita na siku naombewa nilikutwa na mapepo mengi sana na hata waombeaji wakashangaa. Ningejua ningeokoka tangu nikiwa na miaka 5 lakini ndio hivyo sina jinsi wala uwezo wa kubadirisha hali hiyo.

Na naomba kila atakayesoma ujumbe huu ajue kuanzia leo kuwa pombe ni dhambi pia kwenda disko ni dhambi,kuuza pombe ni dhambi na kila kichochoe chochote cha dhambi ni dhambi. Hadi sasa mtu yeyote hawezi kujua kama nina UKIMWI na sijui MUNGU ana mpango gani na mimi maana kwake yote yanawezekana. Nauamini uponyaji wake na sijawahi kutumia ARV hata siku moja na afya yangu iko sawa tu na huwezi hata wewe kujua kama uovu huu nimefanya mimi.

Ndugu zangu kama una UKIMWI nenda kanisani ukaombewe na kama una akili mpe YESU maisha yako maana pia baada ya kifo ni hukumu. Yasalimishe maisha yako kwa YESU na usiambukize wengine tena.

Mimi tangu niokoke sijawahi kufanya mapenzi tena na sitafanya hivyo wala sitaolewa na mtu yeyote maana yatosha kwa uovu niliofanya na hadi sasa wapo ninaowajua zaidi ya 15 wameshafariki na nilihudhulia misibani huku nikijua kabisa chanzo ni mimi.

Mwisho nawashauli wababa kulidhika na wake zao na wamama pia lidhikeni na waume zenu, vijana ambao hamjaoa wala kuolewa subiri hadi utakapooa au kuolewa na kabla ya kuolewa au kuoa kapimeni kwanza kwani wenye UKIMWI ni wengi kuliko unavyozani.

Fuata unachofundishwa kanisani na pia soma BIBLIA na uwe mtakatifu.

MUNGU akubariki

Ni mimi Jane,
Mwenge, Dar es salaam
Tanzania

 
Tuesday, 23 April 2013 14:53 Al Love+Relationships
Print PDF

Kaka amfundisha dada yake ‘kitchen party’ kitandani

Katika siku za mwanzo tu uhusiano wao, Martha alimpa utambulisho boyfriend wake Jacob: “Sweetheart, huyu ni rafiki yangu anaitwa Roy, ni mshkaji wangu wa karibu, mimi na yeye ni kama kaka na dada, siri yangu yake, yake yangu. Baadaye ukiniona naye usije kunionea wivu.”

Jacob aliitikia kisha maisha yakaendelea. Penzi likakua, Jacob alimvalisha Martha pete ya uchumba baada ya utambulisho kwa wazazi kufanyika na kukubalika. Taratibu za ndoa zikashika kasi lakini kuelekea kuoana, kuna jambo la kushangaza likajionesha.

Siku moja asubuhi, Jacob alifika nyumbani kwa Martha kwa ajili ya kumpelekea matumizi. Alikukuta mlango wa sebuleni upo wazi, akaingia na kupitiliza kabisa chumbani. Akastaajabu kumkuta Roy amelala, amejiachia kitandani.

Jacob akasalimia: “Kaka mambo vipi?”

Roy akajibu: “Safi kabisa bro.” Namna Roy alivyojibu, alionesha kujiamini kupita kiasi. Mara, Martha naye akatokea choo cha chumbani akiwa amejifunga kanga moja tu!

“Waooo baby umenisapraiz leo asubuhiasubuhi,” Martha alisema.

Jacob akamtoa Martha sebuleni ili wazungumze. Ile wanaketi tu, Martha akalianzisha: “Baby usishangae kumkuta Roy hapa, aligombana na mkewe, kwa hiyo ikabidi aje alale hapa.”

“Kwa nini aje alale hapa tena kitandani kwako kabisa?” Jacob aliuliza.

“Ndiyo sweetheart, si unajua Roy anavyonipenda na kunizoea mimi dada yake? Ikabidi aje alale hapa, vinginevyo labda angekwenda kulala hotelini, sasa gharama za nini?” Martha alijibu kwa mtindo wa kuhoji.

“Ukaingia chooni kuoga, ukatoka na kanga moja mbele ya Roy, eti kaka yako. Unawezaje kunishawishi nikuamini kuwa wewe na yeye siyo wapenzi?” Jacob aliuliza.

Martha alijitetea, Jacob akamwambia amemwelewa. Alimkabidhi fedha za matumizi kisha akaaga kuondoka. Martha alimsindikiza, akahakikisha Jacob anaingia kwenye gari na kuanza kuondoka ndipo naye akaingia ndani.

Jacob hakufika mbali, alipoangalia kwenye vioo (side mirrors) na kumuona Martha anarudi ndani, aligeuza gari. Alipofika alipaki na kuanza kutembea kwa kunyata. Mlango wa sebuleni alikuta upo wazi, akapitiliza mpaka mlango wa chumbani.

Pale kwenye mlango wa chumbani, akasikia sauti ya Roy ikiuliza: “Vipi jamaa yako ameondoka?”

Martha akajibu: “Bwege yule ameshaondoka, ila kaniuliza maswali magumu? Inaonekana ameshaanza kutushtukia.”

Jacob aliposukuma mlango, aliwakuta Martha na Roy wamelaliana. Walipomwona walishtuka sana, mwenyewe akawaambia: “Endeleeni starehe zenu, mimi bwege nilikuwa napita tu!” Baada ya hapo akaondoka zake.

Kuanzia siku hiyo, Jacob alipokea SMS mfululizo kutoka kwa Martha na Roy wakimwomba msamaha kwa waliyomtendea lakini hakujibu hata moja. Walipiga simu lakini hakupokea. Upande wa pili, Martha alimtupia lawama Roy: “Ona umeniharibia ndoa, nitafanya nini mimi na wewe una mke wako?”

Baada ya wiki tatu, Jacob aliwaita Roy na Martha nyumbani kwake ili waende wakazungumze na kuyamaliza. Walienda haraka sana. Walipofika sebuleni, Jacob aliwaambia waende mpaka chumbani. Haikuwa shida, Martha anakijua chumba, kwa hiyo wakaingia.

Mbona ilikuwa sinema? Jacob alikuwa amelala akiwa amemkumbatia mwanamke mrembo anayeitwa Rosemina. Huyo Rosemina ni mke wa Roy. Palepale Roy na Martha waliteleza na kujikuta wamekaa chini kwa mshtuko. Picha ilikuwa wazi kuwa Jacob na Rosemina ni wapenzi, maana hata pale kitandani hawakuwa na nguo iliyowasitiri.

Jacob akafunguka: “Nyie si mlisema mimi ni bwege, sasa nimeamua kuwaonesha ubwege wangu, kuanzia sasa ninyi nendeni mkaone, mimi nitamuoa Rosemina wangu hapa. Nimempata kwa urahisi kwa sababu naye alikuwa ameshachoshwa na tibia zenu, mnajifanya kaka na dada kumbe mahasidi wakubwa. Na mimi huyu ni dada yangu na hapa namfundisha ‘kitchen party’ ya kitandani.”

 
Tuesday, 23 April 2013 14:42 Al Lifestyle+Fashion
Print PDF

Wema akata tamaa ya maisha

Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu, amekata tamaa ya maisha kufuatia matukio mfululizo yanayomuandama.

Wema, kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram, aliandika kuwa anaamini atakufa na kuacha maneno mengi ya kumuongelea kwa mazuri.

Kuhusu kile ambacho Wema amekisema, soma ujumbe huo katika picha kama ulivyonakiliwa kwenye akaunti yake ya Instagrama.

 
Tuesday, 23 April 2013 14:37 Al Political Issues
Print PDF

Komedi bungeni; bunge nyumba ya mipasho, ubabe

Je, ni sahihi kutumia mabilioni ya shilingi kufanya uchaguzi halafu wanaochaguliwa badala ya kufanya kazi ya nchi, wanakwenda kutukanana, kuoneshana ubabe, kushabikia vyama vyao? Kuna haja ya kufanya tathmini upya.

Je, fedha zinazotumika kuendesha bunge, zinazolipa mishahara wabunge na posho, kazi yake ndiyo hii ya kupigana mipasho na kukifanya chombo hicho muhimu cha kutunga sheria, kiwe mahsusi kwa ajili ya kuoneshana ubabe na ufundi wa kuzungumza maneno machafu ya mtaani?

Utovu wa nidhamu bungeni unazidi kushamiri. Taswira ya sasa, inasherehesha ukweli kwamba bunge limepungukiwa maadili. Na kwa vile wanaounda chombo hicho ni watu, wao ndiyo watovu wa maadili. Bunge makini linajengwa na wabunge makini na kinyume chake.

Yaani, bunge la sasa na matukio ya ‘komedi’ ambayo yanaendelea ni matokeo ya kuwa na wabunge wa aina hiyo. Na hayo ndiyo mazao ambayo tuliyapanda wakati wa uchaguzi. Ni utovu wa busara kutarajia kuvuna mpunga kwenye shamba ambalo wewe mwenyewe ulipanda matembele.

Ni ukweli kuwa yapo makosa ya wapigakura katika kile walichokipanda, yaani wakati wa kampeni hawakufanya kazi nzuri ya kuchagua mbegu bora, wao waliona bora mbegu. Hili linaweza kuwa fundisho kubwa sana katika uchaguzi wowote ujao. Tutajicheka mno tukirejea kasoro hizi.

Hata hivyo, kwa namna pana kabisa, wabunge wenyewe wanajidhalilisha. Kama hawana habari, basi ukweli ni kwamba mitaani kwetu wanawapuuza kwelikweli. Picha ambayo wanawatafsiri, hawawachukulii kama wawakilishi wa kweli, bali makada wa vyama vyao, walioamua kwenda kutetea maslahi yatokanayo na sera za vyama vyao.

Je, bungeni tumewapeleka wabunge kwenda kutetea maslahi ya vyama au kujenga taifa imara lenye maendeleo? Kwa mwendo wa sasa, ni vigumu sana kuona mijadala makini ikichukua nafasi kwa sababu fujo zinatawala. Jazba na hisia za kibinadamu zinawatawala na kuvuruda weledi.

Mbunge anaposimama na kusema “Sizungumzi na mbwa, nazungumza na mwenye mbwa”, huyo anakuwa ametoka nje ya maadili. Mwingine anapotukana kabisa, inasikitisha sana. Naomba niandike kwa msisitizo kuwa aibu iwe kwake Mbunge wa Kigoma Mjini (CCM), Peter Serukamba na tusi aliloliporomosha bungeni.

Serukamba alitukana lakini ni wengi tu ambao walizungumza lugha zisizo na staha. Imekuwa aibu kiasi ambacho, kuna tamko linatolewa kwamba wazazi wanawazuia watoto wao kutazama bunge kwa sababu wanaweza kujifunza lugha zisizofaa. Sijawahi kuona aibu nzito kama hii!

Kwa tafsiri ni kwamba bunge linaonekana ni X, kwa hiyo watu wenye umri chini ya miaka 18, hawatakiwi kabisa kutazama. Sidhani kama kuna fedheha nzito kuliko hii. Hatupaswi kuacha hili liendelee. Kwa maneno na vitendo, tunapaswa kuweka wazi hisia zetu kwa namna ambavyo tunachushwa na komedi za ndani ya bunge.

Unaangalia kikao cha bunge, Televisheni ya Taifa, inakwepesha kamera na baadaye kukatisha kurusha matangazo ili vioja vya ndani ya bunge visionekane. Nashindwa kusadiki kile nilichokuwa nakiamini sana huko nyuma kwamba wabunge ni watu daraja la juu kabisa ambao sauti zao ni ukombozi wa mwananchi.

Kwa maneno ni sawa lakini hali halisi kwa sasa ni tofauti. Tangu Bunge la Bajeti la mwaka wa fedha 2013-2014 lianze, kila siku malumbano. Spika wa Bunge, Anne Makinda anakemea leo, kesho mheshimiwa mwingine anarudia madudu yaleyale yaliyokatazwa. Huu ni zaidi ya utoto.

Mbunge hajaruhusiwa kuzungumza, akiwa ameketi anapaza sauti kupinga hoja ya mwenzake anayezungumza. Bunge linageuzwa soko, mazungumzo yanafanyika bila utaratibu, kila mteja na muuzaji wake, wanaelewana kivyao. Mtu anaitwa baba, tena kiongozi wa wananchi, mwakilishi lakini anafanya mambo ambayo wanafunzi wa shule za msingi wana afadhali.

Upande wa pili, kiongozi wa vikao anapozidiwa na hisia za kibinadamu ni hatari sana. Kila siku narudia kile kipande ambacho Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, aliamuru Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu aondolewe nje ya ukumbi Aprili 17, mwaka huu, napata shida mno.

Pengine Lissu ni mtukutu lakini siku ile alikosea nini? Aliomba mwongozo kama kanuni zinavyomtaka. Ndugai akachukizwa na hilo, akadai anasimamasimama sana. Mbona ilikuwa rahisi tu kumzimia ‘maikrofoni’ au kumwambia akae na kuzuia mwongozo mpaka aliyekuwa anazungumza amalize?

Hisia zilitawala na kupoka hekima na weledi, ubabe ukatawala ndiyo maana wabunge wengine wa Chadema, walisimama kuwazuia askari wasimtoe Lissu nje ya ukumbi. Je, hivyo ndivyo tunapaswa kwenda? Kuna makosa makubwa ya wabunge na baadhi ya viongozi wa vikao.

 
Tuesday, 23 April 2013 14:22 Al Music
Print PDF

Lady Jaydee: Mungu si Ruge wala Kusaga

Stadi wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ ametamka kwamba anaamini hatarudi nyuma na hatatetereka kimuziki kwa sababu anamtumaini Mungu.

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii ya Twitter, Jaydee a.k.a Binti Komando, aliandika: ‘Mungu siyo Ruge wa Kusaga kwa hiyo naamini nitashinda.”

Kabla ya hapo, Jaydee ak.a Jide ambaye zamani alipenda ajulikane kama Binti Machozi, aliandika: “Msemo wa Mungu siyo Athumani kila mtu anaujua, ila mimi ninao mpya.”

Baada ya muda mfupi ndipo akaandika: “Msemo wangu naamini Mungu siyo Ruge wala Kusaga, kwa hiyo naamini nitashinda.”

Jide ambaye ni mmoja wa wanamuziki waasisi wa Bongo Fleva, ameamua kujiweka wazi kiharakati, akipingana na unyonyaji wambao unafanywa katika muziki na washikadau.

Jide kama ambavyo kaka zake wa Vinega walivyokuwa wanafanya katika mixtape za Anti Virus, anawashambulia wakurugenzi wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba pamoja na kituo chao cha redio cha Clouds FM.

 
Thursday, 18 April 2013 06:41 Al Music
Print PDF

Kweli Bi. Kidude ametutoka

Mwanamuziki mkongwe wa Taarab, Fatuma Binti Baraka Khamis,  maarufu kwa jina la  Bi Kidude amefariki dunia leo huko Bububu Zanzibar, sehemu alikokuwa anauguzwa.

Taarifa hizo, zinafuatia uvumi wa mara kwa mara kwamba Bi. Kidude hatunaye lakini nyakati zote zilikuwa uzushi ila sasa ni ukweli kwamba mkongwe huyo ametutoka.

Habari zinasema kuwa, mwili wa marehemu Bi. Kidude, utahamishiwa nyumbani kwake Rahaleo na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho.

Sababu ya kifo chake haijawekwa wazi lakini ukweli ni kwamba Bi. Kidude alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kisukari kwa muda mrefu na tangu mwaka jana, hali yake ilikuwa tete sana.

Vilevile, zipo taarifa kwamba Bi. Kidude alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya uvimbe kwenye kongosho.

Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo, alikuwa binti wa mchuuzi wa nazi, hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe ngapi, wapo wengine wanaoamini kwamba mpaka mauti yamemfika, kulikuwa na uwezekano alishafikisha zaidi ya umri wa miaka 102.

Katika mwaka 1920 tayari alikuwa amekwisha anza kuimba katika vikundi vya sanaa kule kwao, mwaka 1930 alijiunga na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam na kuzunguka miji mingi ya Tanzabua Bara, mwaka 1940 alirudi Zanzibar ambako awali alikuwa amekimbia kwa kuwa aliozwa kwa nguvu na mtu aliyemzidi sana umri.

Bi Kidude pia aliwahi kuimba na Sitti Binti Saadi wakati wa ujana wake  na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni.

Na kuhusu kuzaa, haijawahi kuripotiwa popote kama Bi. Kidude aliwahi kuzaa.

Mungu Amlaze Pema Peponi Bibi yetu. Amen.

 
Thursday, 18 April 2013 06:38 Al Sports News
Print PDF

Niyonzima atoa masharti kabla ya kusaini Yanga

Baada ya kukubali kusaini mkataba na Klabu ya Yanga, kiungo mchezeshaji Haruna Niyonzima sasa ametoa masharti mazito kwa viongozi wa timu hiyo ili amwage wino.

Hivi karibuni Niyonzima alisema kuwa yupo tayari kuongeza mkataba wake Yanga unaotarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Mpaka sasa yupo kwenye mazungumzo na viongozi wa timu hiyo.

Niyonzima, raia wa Rwanda, amesema kuwa, amewapa viongozi wa timu hiyo masharti ili aendelee kuichezea klabu hiyo na kama wasipoyatekeleza hawezi kuongeza mkataba.

Hata hivyo, kiungo huyo aliyetawala safu ya kiungo ya Yanga, amekataa kuyataja masharti hayo, akidai atakuwa tayari kulizungumzia suala hilo baada ya ligi kumalizika.

“Nipo kwenye mazungumzo na viongozi wa Yanga juu ya mkataba mpya. Bado sijasaini. Nimetoa masharti kwa viongozi hao ili nibaki. Nataka waboreshe baadhi ya mahitaji yangu yaliyoandikwa kwenye mkataba,” alisema Niyonzima.

 
Thursday, 18 April 2013 06:29 Al Love+Relationships
Print PDF

Jokate amcheka Uwoya kupitiwa Diamond

Mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, ameangua kicheko baada ya kusikia mwigizaji Irene Uwoya kunaswa hotelini na Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Jokate aliangua kicheko hicho juzikati jijini, Dar wakati alipozungumza na ripota wetu na alipogusiwa kuhusu suala la Uwoya kunaswa na Diamond, alicheka sana huku akimshangaa.

“Hahaha sasa ndiyo nini tena, yeye si aliwahi kunisema mimi nakwapua mabwana? Sasa leo imetokea kwake tena!” alisema Jokate.

Aliongeza: “Kumbe yale yalikuwa maneno maneno, mwisho nay eye ametoka na Diamond, kwa kweli inachekesha sana. Naona kama sinema vile.”

Machi 25, mwaka huu, Diamond na Uwoya, walinaswa kwenye hoteli moja yenye hadhi ya nyota tano, iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam.

Ilielezwa kuwa Diamond na Uwoya, walilala kwenye hoteli hiyo, chumba namba 208, wakiingia saa 8:24 usiku kisha wakatoka kati ya saa 9:00 na saa 9:13 mchana.

 
Thursday, 18 April 2013 06:22 Al Lifestyle+Fashion
Print PDF

Wastara wa Sajuki apata pigo lingine

NI pigo juu ya pigo kwa staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma ambaye miezi minne iliyopita alifiwa na mumewe, Juma Juma Kiwoloko na sasa amepatwa na msiba mwingine mkubwa.

Msiba huu wa sasa umemfanya Wastara kulazwa jijini Dubai baada ya kupata mshtuko kufuatia mdogo wake wa kiume, Abdulmalik  kupigwa risasi na kufariki dunia jijini Dar.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea usiku wa manane, kuamkia Aprili 11, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Lango la Jiji Magomeni Mikumi wakati Abdulmalik alipokuwa akiamua ugomvi kati ya dada yake aitwaye Hawa na shemeji yake aliyejulikana kwa jina la mzee Lyimo.

Kwa mujibu wa mdogo wa marehemu aitwaye Nuru, marehemu siku ya tukio alikuwa nyumbani kwao Magomeni Mikumi na  ilipotimu saa sita usiku alipigiwa simu na Hawa akimuomba aende kumchukua katika Ukumbi wa Lango la Jiji ili warudi nyumbani.

“Wakiwa katika ukumbi huo, muda mfupi baadaye alitokea mzee Lyimo ambaye ana uhusiano wa kimapenzi na Hawa na kuanza kumvamia na kumpiga mwanamke huyo.”

Nuru alisema kuwa kipigo hicho kiliwashtua watu wengi waliokuwa katika eneo hilo na kumfanya Abdulmalik kuingilia ili kuamua ugomvi huo na kumuokoa dada yake asiendelee kupigwa.

“Baada ya kuona hivyo, mzee Lyimo alichomoa bastola na kupiga hewani kuwatawanya watu, wakati Abdulmalik alipokuwa akiamua risasi moja ikampata tumboni,” alisema Nuru kwa masikitiko.

Nuru alidai kwamba baada ya Abdulmalik kupigwa risasi, alipatwa na kiwewe na kuanza kukimbia hadi nyumbani, kisha akajifungia ndani, baadaye akamwambia kaka yake mwingine kwamba alipigwa risasi ya tumboni na shemeji yao.

Binti huyo aliendelea kusema kwamba wakati ndugu hao wakijadiliana, mzee Lyimo alifika nyumbani hapo na kumchukua Abdulmalik kisha kumpeleka katika Hospitali ya Mikumi. Alipomfikisha, alitoweka na kumuacha kijana huyo hospitali hapo.

“Kwa kweli alikuwa katika hali mbaya, ndugu tukaamua kumpeleka Muhimbili lakini tukiwa njiani, Abdulmalik alifariki dunia,” alisema Nuru na kuanza kulia.

Dada huyo alisema kuwa madaktari wa Hospitali ya Mikumi katika uchunguzi wao walibaini kwamba risasi iliyokuwa imempata Abdulmalik ilikuwa imepanda kutoka tumboni na kufika kifuani.

“Yaani kiukweli kifo cha kaka Abdulmalik kinaumiza, ndugu hawaamini na hatujui hali ya Wastara ambaye amelazwa baada ya kupatwa na mshtuko pale tulipompa habari hizi,” alisema Nuru.

Ripota wetu alijaribu kuwasiliana na Wastara kwa njia ya simu, hata hivyo staa huyo alisema kuwa alikuwa katika hali mbaya kutokana na msiba huo na kulazwa kwa mapumziko hivyo asingeweza kuongea vizuri mpaka atakapokuwa sawa.

“Siwezi kwa kweli… naomba niache, nimelazwa kwa mapumziko…” alisema kwa sauti iliyoonesha kwamba alikuwa akilia.

 

 
Thursday, 18 April 2013 06:14 Al Political Issues
Print PDF

Fast Jet: Hata mtu wa chini kabisa sasa anaweza kupanda ndege

Unaweza kutafuta kitu ambacho kinaweza kukufanya usisafiri na Fast Jet kwa sasa lakini ikashindikana. Hii ndiyo kampuni inayotoa huduma bora zaidi na nafuu za usafiri wa anga nchini.

Haina muda mrefu sana tangu ilipojikita kwenye ardhi ya Tanzania lakini ndani ya kipindi hicho kifupi, imeweza kuondoa ile dhana kuwa usafiri wa ndege ni kwa ajili ya watu wenye vipato vya juu.

Aprili 10, mwaka huu, mwanadishi wa makala haya, alisafiri na Fast Jet kati ya Dar es Salaam, Kilimanjaro na Zanzibar na kuzungumza na abiria 27 na kila mmoja alitoa maoni chanya, kuhusu mapinduzi makubwa yaliyofanywa katika Nyanja ya usafiri wa anga na kampuni hiyo ya ndege.

“Niliwahi kusafiri kwa ndege karibu miaka 17 iliyopita. Baada ya hapo sikuwahi kupanda ndege kabisa kwa maana niliona ni gharama kubwa ambazo sikuweza kuzimudu,” alisema Neyman Ndelijwa, 46, mkazi wa Arusha.

Neyman ambaye alikuwa kwenye ndege akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia), akielekea Dar es Salaam, alimweleza mwandishi wa makala haya: “Sasa naweza kupanda ndege, Fast Jet wamerahisha sana maisha ya usafiri.

“Ukiangalia bei ambayo nimelipa, haitofautiani sana na gharama za kawaida za usafiri wa mabasi. Naamini kwamba hivi sasa kila anayesafiri kwa basi, anaweza kupanda ndege na ikawa nafuu zaidi kupitia Fast Jet.”

Anachokizungumza Neyman ni kweli kabisa, kwani mapinduzi ya sasa ya Fast Jet, yanafanya usafiri wa ndege kuwa gharama nafuu mno kupita hata basi.

Mathalan; kwa usafiri wa basi kwenda Mwanza, nauli ni kati ya shilingi 45,000 mpaka 60,000. Fast Jet yenyewe inatoza nauli ya chini kabisa shilingi 43,000, yaani usafiri shilingi 32,000 na kodi shilingi 11,000, jumla shilingi 43,000.

Vilevile unapopanda Fast Jet, haikulazimu kuingia gharama za ziada kwa ajili ya matumizi ya njiani. Kati ya dakika 45 na 60, unakuwa umeshafika unapokwenda.

Unaposafiri na basi, mbali na kutumia saa nyingi njiani, vilevile itakulazimu kununua chakula kuanzia asubuhi, mchana na wakati mwingine jioni, kwani unakuwa bado hujafika. Kwa kifupi, Fast Jet ni mkombozi wa kila Mtanzania.

Hakuna sababu ya kutumia saa nyingi njiani au wakati mwingine kupitisha zaidi ya siku ukisafiri, eti kwa kukimbia gharama za kusafiri kwa ndege, wakati Fast Jet inakusafirisha kwa bei nafuu kuliko hata ile ambayo ungelipa kwa basi.

Musika Nyangabo, 41, aliyekuwa anatokea JNIA kwenda Kia, alisema: “Fast Jet ni nafuu sana. Mimi na mtoto wangu tumeweza kusafiri kwenda na kurudi, Kilimanjaro – Dar kwa shilingi 282,000. Unadhani kama ingekuwa ni kwenye makampuni mengine hali ingekuwaje? Nafurahia bei na huduma za Fast Jet.”

NI HUDUMA KAMA ULAYA

“Ni mara yangu ya kwanza kuja Tanzania, Watanzania wana kila sababu ya kujivunia Fast Jet kwa sababu ni kampuni bora sana ya ndege,” alisema Okite Obakponovwe, 37, raia wa Nigeria ambaye alizungumza na mwandishi wa makala haya, akiwa angani kutoka Kia kwenda Julius Nyerere International Airport, Dar es Salaam.

Mnigeria huyo, aliyekuwa Kilimanjaro kwa ajili ya kutalii Mlima Kilimanjaro, aliongeza: “Fast Jet ni sawa na Kampuni ya Easy Jet ya Uingereza. Kila huduma inayotolewa na Fast Jet, inaendana na Easy Jet, kwa kifupi Tanzania imepata bahati kuliko nchi nyingine yeyote Afrika.

Obakponovwe ambaye alikuwa ameongozana na mkewe, Irene Okite, aliongeza: “Gharama ni nafuu sana. Hata kule Uingereza Easy Jet ni nafuu. Mimi na mke wangu, tumefurahia huduma za Fast Jet, tumeweza kusafiri vizuri na ndege zake zina uhakika wa safari na kufika salama kwa asilimia 100.”

Abiria wengine waliozungumza na mwandishi wa makala haya ni Faraja Temu, aliyewasili Uwanja wa Ndege wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Karume, Zanzibar akitokea Kilimanjaro, yeye alisema: “Nafurahia huduma, Fast Jet imerahisha maisha yetu ya usafiri hata kwetu sisi wanafunzi.”

NDEGE ZA AIRBUS BORA SANA

Mhudumu wa ndege, Jasmine Kaungu, alisema: “Nilishafanya kazi kwenye makampuni tofauti ya ndege hapa nchini, ila najisikia fahari kufanya kazi na Fast Jet. Abiria wanasafiri kwa uhakika sana kutokana na ndege zetu aina ya Airbus ambazo ni bora sana.”

Mmoja wa wasimamizi wa huduma kwa wateja, Omar Chinguile, alisema: “Kikubwa kwetu ni umakini. Menejimenti yetu ipo makini kuhakikisha wateja wanapata huduma bora sana. Ripoti yoyote inayoonesha uzembe, husababisha mfanyakazi apoteze ajira.”

BOOKING YA MAPEMA NI MUHIMU

Mkuu wa Oparesheni wa Fast Jet, Kia, Robert Kessy alisema: “Nashauri abiria wawe wanajitahidi kufanya booking mapema ili wapate bei ya chini kabisa ambayo ni shilingi 43,000. Wanapochelewa ndiyo hukutana na bei za juu. Kwa kawaida bei zetu zinaanzia shilingi 43,000 mpaka shilingi 300,000.”

CAPTION:

1. Abiria wakipanda ndege ya Fast Jet, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, wakielekea Kilimanjaro, Aprili 10, mwaka huu.

2. Abiria wakiwa ndani ya moja ya ndege za Fast Jet, iliyokuwa inatokea Dar es Salaam kwenda Kilimanjaro.

3. Okite Obakponovwe, raia wa Nigeria, akiwa ndani ya ndege ya Fast Jet, yeye alieleza kwamba huduma za Fast Jet ni bora sawa na zile za Easy Jet ya Uingereza.

4. Mkuu wa huduma za ndani ya ndege katika moja ya ndege za Fast Jet, Omar Chinguile (kushoto), akizungumza na mwanadishi wa habari na mmiliki wa Blogu ya Full Shangwe, John Bukuku, wakati wakiwa safarini kutoka Kilimanjaro kwenda Zanzibar, Aprili 10, mwaka huu.

5. Marubani wa Fast Jest, John Lewis (Kushoto) na Alex Taylor (katikati), wakiwa na mhudumu wa ndege, Jasmine Kaungu, muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kutoka Kilimanjaro kwenda Zanzibar, Aprili 10, mwaka huu.

 
Thursday, 18 April 2013 06:04 Al Music
Print PDF

Bosi wa East Africa Melody afariki dunia

Mkurugenzi wa Kikundi cha Taarab cha East African Melody, Hadji Mohamed, amefariki dunia asubuhi hii baada ya kuugua kwa muda mfupi katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Taarifa zaidi kuhusu kifo hicho, zitakuja baadaye.

 
Thursday, 11 April 2013 11:07 Al Lifestyle+Fashion
Print PDF

Beckham adaiwa kukuza nyeti

Kiungo wa PSG, David Beckham, amedaiwa kuchoma sindano ya kukuza maulile yake nyeti ili awe mkali zaidi kunako uwanja wa faragha.

Kwa mujibu wa gazeti moja la England, Beckham ‘alibusti’ nyeti zake kwa sindano, lengo kupata mwonekano mzuri hata anapovaa nguo za ndani ya boxer.

“Kila kitu kuhusu Beckham na alichofanya kukuza ukubwa wa nyeti zake, kinajulikana,” kilisema chanzo cha habari. “Kwa kipindi hiki anavaa boxer kwa ajili matangazo, namna anavyoonekana sasa akiwa na boxer, ndivyo alitaka na sasa imekuwa.”

Inadaiwa kuwa kiungo huyo mwenye heshima kubwa England, aliwahi kushauriwa kufanya upasuaji lakini mwenyewe aligoma na akataka achomwe sindano, kitu ambacho kilifanyika.

Imebainishwa kuwa Beckham anakuwa mmoja wa wanaume wa England na Uingereza yote kwa jumla ambao wamefanya mambo mbalimbali kuhakikisha wanakuza nyeti zao.

Inazidi kuelezwa kuwa wanaume wa Uingereza, wapo radhi kutoa fedha nyingi ili wafanyiwe upasuaji au kuchomwa sindano waweze kukuzwa nyeti zao kwa imani kuwa zinawaongezea mvuto wa kimapenzi kwa wanawake.

“Itabidi uchunguzi ufanyike, ni kwa nini sasa hivi wanawake wengi wa Uingereza wawe wanataka sana maumbo makubwa ya nyeti za wanaume. Huko nyuma hakukuwa na hisia hizi, kila mmoja aliridhika na umbile lake lakini sasa ni shughuli,” alisema.

 
Thursday, 11 April 2013 11:04 Al Political Issues
Print PDF

Tunamchekea gavana Bot halafu tunalia kupanda kwa nauli

Mfumuko wa bei ni janga kubwa. Tafsiri yake tu inatosha kuonesha namna ambavyo hatupaswi kuuchekea. Kama taifa, tunateseka leo kwa sababu ya kushindwa kuudhibiti. Wananchi wa chini wanaangamia.

Maana yake ni kupanda kwa gharama za maisha. Bei za vitu na huduma muhimu za kijamii zinakuwa juu. Wakati mwingine ni matokeo ya kushuka thamani ya sarafu. Ulegevu wa benki kuu au udhaifu wa wizara ya fedha na uchumi katika usimamizi wa utekelezwaji wa bajeti, kwa tafsiri iliyooka, ndiyo kitovu cha tatizo.

Wiki iliyopita, Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), ilitangaza bei mpya ya nauli. Michango ya wengi, inaonesha kuwa ongezeko la gharama za usafiri siyo mwafaka, kwani ni nyundo nyingine kwa wananchi wa tabaka la chini.

Sumatra imetangaza kuwa sasa nauli zitapanda kwa asilimia 24.46 (kadiria asilimia 24.5), kwa hiyo mwananchi aliyekuwa anapanda daladala kwa shilingi 300, sasa atalipa shilingi 375 (kadiria 400). Msafiri wa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine, aliyelipa shilingi 40,000, sasa atatakiwa alipe shilingi 50,000.

Ni mpanga bei anayepitiwa na msemo “mwenye shibe hamkumbuki aliye na njaa” ndiye peke yake anayeweza kuona bei hizi ni rahisi. Watanzania wanateseka, kuendelea kuwapandishia gharama za maisha ni kuzidi kuwaumiza na kuwakatisha tamaa.

Mfumuko wa bei ukiendelea kuitesa nchi, ajabu ni kwamba Gavana wa Bot, Benno Ndullu bado yupo palepale. Ufanisi wake hauonekani katika kuhakisha  benki kuu kama roho ya nchi, inafanya kile kinachotakiwa kuhakikisha gharama za vitu muhimu na huduma nyeti, hazipandi.

Taarifa kwamba mfumuko wa bei umefikia asilimia 20, inatoa picha kuwa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2012-2013, imepunguza uwezo wa kununua bidhaa na huduma kwa takribani asilimia 6. Hii ni sawa na shilingi trilioni moja kuyeyuka kabla hata mwaka mpya wa fedha haujafika.

Hali ni mbaya zaidi kwa wananchi, kwani mfumuko wa bei za vyakula umekua kwa kasi kikubwa mno. Ofisi ya Takwimu ilishaonesha kuwa mfumuko wa bei za chakula pekee umepaa kwa wastani wa asilimia 25. Upande huo kukiwa bado majanga, nauli nazo zinaongezeka.

Hata hivyo, ukiangalia kwa undani zaidi, utakuja kugundua kuwa bei za chakula zimekuwa maradufu, ukilinganisha na hali ilivyokuwa miaka miwili iliyopita. Mchele, sukari, nyama, samaki, sembe na ngano, vyote vimepanda kwa kati ya asilimia 30 mpaka 50.

Gesi ipo juu, mafuta ya taa yalishapanda kwa asilimia 71 mpaka 75 tangu miaka miwili iliyopita. Hii inasababisha wengi wakimbilie nishati ya mkaa ambayo ni hatari, ingawa nako huko ni pagumu kwa mwananchi wa kawaida, kwani umepanda kwa asilimia 30.

Mfumuko wa bei unasukuma Watanzania wengi zaidi kwenye dimbwi la umasikini, unapunguza uwezo wa serikali kutoa huduma za kijamii kupitia bajeti na hata kutimiza mipango ya miradi ya maendeleo kama miundombinu ya barabara, umeme, bomba la gesi, madaraja nk. Mkakati mahususi unatakiwa kubadili hali hii.

Kwa namna tunavyokwenda, kama tusipochukua hatua, kuna hatari ya dhahiri kwamba tunaweza kurejea mfumuko wa bei wa mwaka 1992 ambao ni asilimia 22, kadhalika tunaweza kuukaribia ule uliokuwa tishio zaidi, wa mwaka 1994, asilimia 33.

Kwa nini Ndullu anastahili lawama na kuwajibishwa kwa hili? Siku zote kuna njia mbili ambazo husimamiwa na benki kuu katika kudhibiti mfumuko wa bei. Mojawapo ni Monetary Measures, hii hugusa moja kwa moja sera kuhusu uchumi ndani ya benki kuu kwa kuweka riba kubwa dhidi ya mabenki ya kibiashara ili kuifanya serikali (hazina) kuwa na akiba nzuri.

Bot lazima isimamie sera ya riba ili kusababisha kupanda kwa gharama za kukopa dhidi ya mabenki ya kibiashara kutoka benki kuu. Matunda yake ni kupungua kwa mtiririko wa fedha kwa wananchi, hilo likifanikiwa serikali itaweza kupanga bei za bidhaa kulingana na hali za wananchi. Hivi sasa fedha zipo nje, wafanyabiashara wana hela sana, kwa hiyo inakuwa vigumu kuwadhibiti.

Mfumuko wa bei kwa tafsiri nyingine ni matokeo ya wafanyabiashara kuizidi nguvu serikali, kwa hiyo wanajipangia bei bila kupingwa. Ndullu kwa nafasi yake, anatakiwa kuhakikisha sera zinafanya kazi, serikali inakuwa na nguvu siku zote dhidi ya wafanyabiashara. Bot ikiendelea kusinzia, stori zitabaki zilezile.

 
Thursday, 11 April 2013 10:57 Al Love+Relationships
Print PDF

Mama alipompa mwanaye huduma ya faragha usiku mzima

Mama Moses ni mwanamke wa kimjinimjini, alianza kuwajua wanaume mapema sana. Akiwa na umri wa miaka 16, alipewa ujauzito na jamaa aliyekuwa kondakta wa daladala kwa wakati huo. Hakuwa na jinsi alijifungua mtoto wa kiume, akamwita Moses.

Kwa sasa Mama Moses ana umri wa miaka 44, Moses ana miaka 28. Mtu na mwanaye wanaishi kama wazungu. Maisha yao si haba, kwani miaka 19 iliyopita, Mama Moses alimliza mzungu mmoja kiasi kikubwa cha fedha, baada ya hapo akawekeza kwenye biashara mbalimbali, ikiwemo maduka Kariakoo na akawa anafuata mizigo China.

Moses ni mtoto wa pekee, kwa hiyo maisha yake yakawa kutumbua fedha za mama yake. Alizitumia kuendesha magari makali akiwa na umri mdogo kabisa. Alihakikisha anatoa ule mkong’oto wa baba na mama kwa warembo tofautitofauti, ikiwemo wanafunzi.

Hakuishia hapo, Moses alibeba mpaka mizigo inayomzidi kimo. Alitoka kimapenzi na wanawake wenye umri kumzidi hata mama yake. “Ninapopata jimama la ukweli, lililonizidi umri nainjoi sana. Hawa watoto nimewazoea, hawanipi stimu kabisa,” Moses aliwahi kumwambia rafiki yake Slay.

Kwa upande mwingine, Mama Moses tangu afikishe umri wa miaka 40, hakutaka kabisa kushiriki mapenzi na wanaume wenye umri mkubwa zaidi yake. “Zamani nilikuwa natembea na mibaba ili nipate fedha, sasa hivi hela ninayo, nataka vijana tu wanipe raha,” hiyo ni kauli ya Mama Moses, akimwambia shosti wake Monica.

“Hivi wewe Moses huwezi kuangalia warembo wa saizi yako? Tabia gani ya kutembea na mimama mikubwa, tena mingine inaweza hata kunizaa,” Mama Moses aliwahi kumwonya mwanaye.

“Mama wewe ndiye unanikata stimu, unatoka na vijana wadogo saizi yangu, wengine hata mimi nawazidi umri,” Moses alimjibu mama yake. Pamoja na hivyo, hakuna kati yao aliyekoma.

Kuna siku moto uliwaka nyumbani kwao. Mama mtu alianza kumtuhumu mwanaye kuwa ametembea na rafiki yake Monica. “Wewe Monica si ni mama yako kabisa? yule ni rafiki yangu wa siku nyingi, wewe unajua lakini umetembea naye bila woga,” Mama Moses alimuwakia Moses ambaye naye alijibu: “Kweli mama mkuki kwa nguruwe, wewe ulifurahi sana ulipotoka na mshakaji wangu Aslay.”

Maisha yalizidi kwenda kasi, siku moja Moses akiwa klabu na marafiki zake, mara Jaca ambaye ni mshakaji wake mwingine aliingia. Walipiga stori mbalimbali lakini katikati ya mazungumzo, mmoja wa marafiki wa Moses alimuuliza Jaca ni kwa nini alichelewa klabu?

Jaca akajibu: “Leo jionijioni nilikutana na bonge la jimama, likanizimia halafu lina mawe kinoma, nikaona siyo vibaya ngoja nijiweke. Tulikula bata, tukaziua bia kama tumerogwa vile, baada ya hapo tukazama zetu chumbani kwenye hoteli moja hapo kati.

“Kabla ya kuanza mambo, machale yakanicheza. Ikabidi nimsimamie yule jimama aendelee kunywa, alewe ili nimtoroke. Alipolewa nikamkimbia zangu ndiyo maana mnaona nimechelewa. Maradhi mengi jamani, ukimwi upo.”

“Acha uzembe wewe, kwani hakuna kondomu?” Moses alimjibu Jaca. Papo hapo akaomba aelekezwe hoteli na chumba ambacho amemwacha huyo bi. mkubwa. Maelekezo yalifanyika, Moses ikabidi ajipe stimu kwa kupiga pombe za kutosha ndiyo amvae jimama aliyeogopwa na Jaca.

Baada ya kujitwika pombe za kutosha, Moses aliongozana na Jaca mpaka hotelini, wakapanda ghorofani mpaka kwenye chumba husika. Jaca aliingia kwanza kuhakikisha mazingira yapo salama, alipojiridhisha, alizima taa, halafu akatoka nje.

“Sasa wewe ukiingia ndani, anza kazi. Mama yupo hoi, usiwashe taa atakushtukia mapema,” Jaca alimpa maelezo Moses ambaye aliyapokea kisha akaingia ndani. Alipofika tu, alisoma gizani na kujua mahali kitanda kilipo na bi. mkubwa akiwa amejaa tele.

Akavua nguo harakaharaka, kisha akahamia kwa yule bi. mkubwa, akamchojoa kiwalo kimoja baada ya kingine. Alipofikia usawa wa kufuli, jimama lilijigeuza kama mzigo kisha akazungumza kwa sauti ya pombe: “Safi baby, unataka kunipa raha.”

Moses wala hakujibu, alichokifanya kwa wakati huo ni kumwandaa bi. mkubwa, tayari kwa shughuli inayofaa eneo walilopo. Jimama akawa anahangaika huku na huko, pombe zikawa zinamezwa na ule mchezo aliokuwa anafanyiwa. Mwisho mechi ikaanza.

Ilikuwa mechi yenye kila aina ya kashkashi za utamu kwa pande zote mbili. Moses alijitahidi kucheza salama, kila baada ya mchakamchaka mfupi, alichomoa daruga kuhakikisha kama kiatu kipo, kimevuka au kimepasuka. Aliporidhika kipo aliendelea kwa ari, nguvu na kasi zaidi.

Baada ya mchuano, wote walipitiwa na usingizi. Palipokucha, mwanga ukiwa umeshaingia chumbani, yaani siyo giza tena, Moses ndiye alikuwa wa kwanza kuamka. Akakumbuka matukio ya usiku uliopita, pombe zilishamwisha, akamwangalia jimama aliyepata naye raha usiku mzima.

“My God,” Moses alijikuta akitamka maneno hayo kwa mshangao. Ni maneno hayohayo ndiyo yaliyomwamsha yule bi. mkubwa ambaye mpaka wakati huo, alikuwa hana nguo hata moja.

Macho yakawatoka wote wawili, hakuna aliyethubutu kufungua kinywa kuzungumza chochote, kwani yule bi. mkubwa hakuwa mwingine, bali ni Mama Moses, kwa hiyo mama na mwana walipeana huduma ya faragha usiku mzima bila kujuana.

 

Page 1 of 2

<< Start < Prev 1 2 Next > End >>